Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari Majaliwa ajitosa ukaguzi mgodi Mirerani
HabariHabari za Siasa

Majaliwa ajitosa ukaguzi mgodi Mirerani

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania
Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema, Serikali imepokea na itayafanyia kazi malalamiko ya wabunge juu ya utaratibu wa ukaguzi unaofanywa kwenye mgodi wa Mererani, mkoani Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Majaliwa alitoa kauli hiyo jana Alhamisi, tarehe 29 Aprili, 2021, wakati akijibu hoja ya Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka ambaye alitaka maelezo juu ya utaratibu wa ukaguzi katika mgodi huo.

Mbunge huyo alikuwa akichangia mjadala wa hotuba makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini.

Mwingine alikuwa ni mbunge wa Geita, Joseph Msukuma aliyesema, ukaguzi umekuwa ukifanyika kwa kuvuliwa nguo, jambo ambalo ni kinyume na utaratibu na unakiuka utu wa mwanadamu.

Majaliwa alisema “nimesikia concern ya namna ukaguzi, unavyoendelea katika mgodi wa Mirerani, nilipanga kutembelea Mirerani ili kuona hali hiyo na kutafuta ufumbuzi, nikuahidi Mhe. Spika na waheshimiwa wabunge, tumepokea na Serikali tutalifanyia kazi.”

Alisema Serikali inapata fedha nyingi kupitia madini ya Tanzanite yanayochimbwa katika mgodi huo hivyo haiwezi kushindwa kununua mtambo unaoweza kufanya ukaguzi wenyewe bila kusumbua mtu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!