Friday , 9 June 2023
Home Kitengo Michezo Majaliwa aipongeza Yanga, aitaka Simba ijifunze
Michezo

Majaliwa aipongeza Yanga, aitaka Simba ijifunze

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Klabu ya Yanga kwa kuichabanga timu ya Marumo Galants kutoka nchini Afrika Kusini jumla ya bao 2-0 na kuweka matumaini ya kutinga hatua ya Fainali ya Kombe la shirikisho barani Afrika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo tarehe 11 Mei 2023 bungeni jijini Dodoma ambapo mbali na kuipongeza amesema wawakilishi hao pekee wa Tanzania, wanaipeperusha bendera ya Taifa vizuri.

“Tunawaombea sana washinde kwa magoli mengi kwani Watanzania tunahamu ya kuona klabu ya Tanzania ikiingia hatua ya fainali.

“Pia niipongeze Simba SC. kwa hatua waliyofikia, tunaamini wamejifunza na kuona kutoka kwa klabu jirani. Tunaamini katika msimu ujao kwenye mashindano hayo tutaingiza klabu mbili au zaidi,” amesema.

Baada ya mchezo wa mkondo wa kwanza wa nusu fainali uliopigwa jana tarehe 10 Mei 2023 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, Yanga inatarajiwa kurudiana katika mechi ya mkondo wa pili tarehe 17 Mei 2023 nchini Afrika Kusini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariMichezo

Benki ya NBC yazindua kombe jipya la Ligi Kuu Tanzania Bara

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa Ligi ya NBC , Benki ya Taifa...

MichezoTangulizi

Yanga malizeni ugomvi na Fei Toto – Rais Samia

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Michezo

Samia aipongeza klabu ya Yanga kwa hatua iliyofikia

Spread the love RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Michezo

Yanga waitwa Ikulu kesho Jumatatu

Spread the love RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kesho Jumatatu, tarehe...

error: Content is protected !!