Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Michezo Majaliwa aipongeza Simba, amwagia sifa Barbara
Michezo

Majaliwa aipongeza Simba, amwagia sifa Barbara

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania
Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameipongeza klabu ya Simba kwa kufanikiwa kuingia hatua ya makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na kupata ushindi kwenye mchezo wao wa kwanza dhidi ya AS Vita kutoka Congo DR. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam …(endelea).

Simba jana ilianza kampeni yake kwenye mchezo wa kundi A, na kufanikiwa kuibuka na pointi tatu kwenye ardhi ya Congo kwa mara ya kwanza baada ya kuondoka na ushindi wa bao 1-0 lilifungwa na Chriss Mugalu dakika ya 60 kwa mkwaju wa penalti.

Katika hotuba yake ya kuhalisha mkutano wa pili, kikao c ha 10 cha Bunge jijini Dodoma, Majaliwa alisema kuwa anaipongeza klabu hiyo kuingia hatua hiyo na kushinda mchezo wake wa kwanza huku hakuwa nyuma kumpongeza mtendaji mkuu wa klabu hiyo Barbara Gonzalez kwa kutangaza utalii kupitia jezi za timu hiyo.

Barbara Gonzalez, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba

“Nitumie nafasi hii kumpongeza Mtendaji Mkuu wa timu hiyo, mwanadada Barbara Gonzalez kwa ubunifu na kushirikisha Wizara ya Maliasili na Utalii na hivyo kulipa heshima Taifa letu kwa kulitangaza kupitia jezi yao kwa maneno VISIT TANZANIA huu ni uzalendo wa hali ya juu ambo unapaswa kupongezwa na kuigwa,” alisema Majaliwa

Simba mabyo kwenye michuano hiyo imepangwa kundi A, sambamba na timu za AS Vita ya Congo DR, Al Ahly kutoka nchini Misri na El Merreikh ya Sudan.

Tayari Simba imeshajikusanyia pointi tatu kibindoni na kuongoza kundi hilo na mchezo unaofuata watakuwa nyumbani kuikaribisha klabu ya Al Ahly, mchezo utakaopigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, tarehe 23 Februari 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

error: Content is protected !!