WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amewahimiza wakazi wa Kigoma na watanzania kuwekeza katika zao la mchikichi na kusisitiza ndio fursa ya kukuza uchumi wa Taifa. Anaripoti Eliabu Kanyika (DSJ) … (endelea).
Majaliwa ametoa wito huo jana Jumapili, tarehe 26 Februari 2023 alipokuwa akizungumza na wawekezaji na wadau wa zao la chikichi mkoani Kigoma.
Katika kutekeleza dhana hiyo ya upandaji wa chikichi amesisitiza uongezekaji wa kasi katika upandaji wa michikichi kwakuwa michikichi ni fursa kwa kila mwananchi.
“Chikichi ni uchumi wa mtu mmoja mmoja na ni uchumi wa Kitaifa,” amesema Majaliwa.
Na pia amesisitiza wazazi kuwarithisha watoto wao uchumi katika zao la michikichi ambalo litawasaidia maishani mwao.
“Kama unataka kumrithisha mtoto mrithishe zao la mchikichi,” amesema Majaliwa.
Leave a comment