Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maige ahoji sababu Tanzania kushindwa kugundua mafuta
Habari za Siasa

Maige ahoji sababu Tanzania kushindwa kugundua mafuta

Spread the love

 

MBUNGE wa jimbo la Uyui nchini Tanzania, Almasi Maige, amehoji sababu ya Tanzania kushindwa kupata nishati ya mafuta licha ya kuwa na viashiria vya mafuta vinavyyofanana na nchi zilizopata mafuta. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Maige amesema jambo hilo limfanya kujiuliza maswali kwamba huenda ni matumizi ya teknolojia duni, hujuma, utaalamu mdogo na kutokuwepo utashi.

Mbunge huyo amehoji hayo leo Alhamisi tarehe 2 Juni, 2022 bungeni jijini Dodoma akichangia hoja ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati.

“Mimi sijui kwanini Tanzania hatujapata mafuta kwasababu wenzetu walikopata mafuta ni ushoroba uleule wa bonde la ufa na hapa kwetu limeanzia hapa. Najiuliza ni teknolojia ndogo ya utafutaji mafuta, utaalamu mdogo, hakuna utashi, hujuma, uwekezaji mdogo na mengine.”

January Makamba, Waziri wa Nishati

Amemtaka Waziri Januari Makamba kulifanyia kazi “Makamba mimi nitakushika wewe kwasababu haya ni mambo yako kahakikishe tunapata mafuta.”

Amesema huko Wembeni Tabora kuna eneo limeonekana lina uwezekana wa kuwa na mafuta lakini uchunguzi ni mdogo unaofanyika “na wataalamu wanaokwenda hawabebi vifaa vikubwa.”

Pia alihoji sababu ya kukifanya kipaumbele cha utafutaji gesi na mafuta kuwa namba 11, “kwanini kisiiwe kipaumbele cha kwanza, hamtaki kupata mafuta?” alihoji.

Katika hotuba yake ya bajeti aliyoiwasilisha bungeni jana tarehe 1 Juni, 2022, Makamba amesema jumla ya vitalu vya kimkakati 11 vilifanyiwa kazi za utafiti wa mafuta na gesi katika mwaka wa fedha 2021/22 na tafiti hizo zipo katika hatua mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!