Thursday , 18 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mahakama yapiga chini marufuku ya kuvaa sketi fupi ‘minisketi’
Kimataifa

Mahakama yapiga chini marufuku ya kuvaa sketi fupi ‘minisketi’

Spread the love

Mahakama ya Katiba nchini Uganda imefuta sheria iliyokuwa imepiga marufuku wanawake na wasichana nchini humo kuvaa nguo fupi kufuatia shinikizo la wanaharakati. Imeandaliwa na Gabriel Mushi, Dar es Salaam … (endelea).

Sheria hiyo ambayo ilipitishwa mwaka 2014, pia ilikuwa inanuia kuzuia usambazaji wa picha za ngono mtandaoni ili kuwalinda wanawake na watoto.

Hata hivyo, waliopinga sheria hiyo walihoji kuwa kanuni hiyo ilitumiwa vibaya na kusababisha wanawake waliovaa nguo fupi kushambuliwa mtaani.

Wakitoa uamuzi wao jana tarehe 18 Agosti, jopo la majaji watano wa Mahakama hiyo kwa kauli moja waliamua kuwa vifungu vya sheria hiyo vinakiuka katiba.

Majaji hao walisema hakutakuwa na madhara yoyote kwa wanawake na wasichana kuvalia mavazi yanayoonyesha maungo yao.

Baada ya sheria hiyo maarufu ‘sheria ya minisketi’ kupitishwa, kulikuwa na maandamano makubwa jijini Kampala kupinga wanawake kufanyiwa ukatili mitaani pindi walipovaa nguo fupi.

Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu walikwenda mahakamani wakitaka sheria hiyo ifutwe na sasa imetupiliwa mbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

Habari za SiasaKimataifa

Rais Faye amteua aliyekuwa mfungwa mwenzie kuwa waziri mkuu

Spread the loveRais mpya wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, amemteua Ousmane Sonko...

error: Content is protected !!