Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mahakama yamkubalia Mdee shingo upande
Habari Mchanganyiko

Mahakama yamkubalia Mdee shingo upande

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imekubali shingo upande sababu za Halima Mdee, Mbunge wa Kawe kushindwa kuhudhuria kesi yake leo 7 Februari 2019. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mdee alitakiwa kuhudhuria kesi yake ya kutoa lugha chafu kwa Rais John Magufuli kwa madai ya kumuuguza mbunge mwenzake Ester Bulaya (Bunda Mjini) mkoani Dodoma. 

Kutoka na taarifa hiyo, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imeshindwa kuendelea kusikiliza kesi hiyo.

Mdhamini wa Mdee, Faris Lupomo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba alitaja sababu hiyo wakati kesi hiyo ilipoletwa kwa ajili ya kutajwa.

Hakimu Simba amesema, sababu zilizotolewa na mdhamini huyo kuhusu kushindwa kufika mahakamani kwa mshtakiwa zinaleta ukakasi na kubainisha kuwa, zina lengo la kuifanya kesi hiyo isimalizike kwa wakati.

Hakimu huyo amesema, madaktari na wabunge wengine wanawake ambao wanaweza kumuuguza Bulaya wapo na kwamba, mahakama ikiruhusu hayo yaendelee kesi itashindwa kumalizwa.

“Kiukweli jambo hili linakwaza na linatia wasiwasi kama hii kesi tutaweza kumaliza kwa mwendo huu, tunakubali sababu hiyo ya kuuguza lakini kwa shingo upande.

Hata hivyo Lupomo amedai, aliwasiliana na mbunge huyo na kumueleza kuwa atashindwa kufika mahakamani kwa kuwa, anamuuguza Bulaya katika Hospitali ya Bunge mkoani Dodoma.

Wakili wa Utetezi Hekima Mwasipu naye alikiri mahakamani hapo kwa mshtakiwa huyo hayupo na amepewa taarifa na mdhamini huyo kuwa, anamuuguza Bulaya mjini Dodoma.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi 28 Februari mwaka huu. Mpaka sasa mashahidi watatu wameishatoa ushahidi katika kesi hiyo akiwemo Mkuu wa Kituo cha Polisi Urafiki, Mrakibu wa Polisi Batseba Kasanga.

Mdee anadaiwa kutenda kosa hilo tarehe 3 Julai 2017 akiwa katika ofisi za Chadema zilizopo Mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Anadaiwa kutamka “anaongea hovyohovyo anatakiwa afunge breki” na kudaiwa kitendo hicho kingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!