AKAUNTI 15 zinazomilikiwa na Mchungaji mtata, Ezekiel Odero, zimeamriwa na Mahakama nchini Kenya kuzuiliwa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Taarifa zinasema, amri ya kuzuia akaunti hizo zilizopo kwenye mabenki tofauti, imekuka kufuatia ombi lililowasilishwa na Ofisi ya Mkurungenzi wa Mashitaka (DCI), mahakamani hapo jana.
Katika waraka uliowasilishwa mahakamani, DCI, ilidai kuwa Mchungaji huyo wa Kanisa la New Life Prayer Centre, anashukiwa kwa utakatishaji wa fedha.
Anatuhumiwa kuwa na uhusiano na Mchungaji wa Kanisa la Good News International, Paul Mackenzie, ambaye anachunguzwa kwa madai ya kuwalaghai wafuasi wa kanisa lake, kufunga hadi kufa ili ‘’kukutana na Yesu.”
Wapelelezi waliiambia Mahakama kuwa akaunti za benki za Mchungazji zimekuwa zikipokea kiasi kikubwa sana cha fedha ambazo zinashukiwa kuwa haramu.
Anasema, mamilioni hayo ya shilingi za Kenya na fedha nyingine za kigeni, zinatoka kwa wahanga ambao wanadaiwa kulaghaiwa kuuza mali zao na kumpatia mchungani Mackenzie.
Wameitaka mahakama kuwaruhusu kuzifikia akaunti kadhaa zilizopo katika mabenki ya Equity Co-op Bank, Kenya Commercial Bank (KCB) na Housing Finance Company Limited (HFC Bank).
Kulingana na afisa wa polisi waanayefanyia uchunguzi DCI, Martin Munene, Jamhuri inahofu kuwa fedha hizo zilizoshikiliwa katika akaunti mbali mbali za benki zitahamishwa iwapo Mahakama haitatoa agizo la kuzifikia akaunti hizo.
Wiki iliyopita, mchungaji Ezekiel alikwenda katika Mahakama ya juu zaidi mjini Mombasa, akitaka kuzuia kufujwa kwa akauntu zake.
Alikuwa amedai kuwa kushikiliwa kwa akaunti zake kutakuwa ni kuingilia uhuru wake na wa kanisa, pamoja na waumini wa kanisa analoliongoza.
Suala hilo linatarajiwa kuendelea kusikilizwa mahakamni kesho Jumanne.
Leave a comment