Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama Kuu yawatosa Mbowe, vigogo wa Chadema
Habari za Siasa

Mahakama Kuu yawatosa Mbowe, vigogo wa Chadema

Spread the love

MAOMBI ya Rufaa ya viongozi wa chama cha Chadema yametupiliwa mbali na Mahakama ya Rufaa kutokana na hati ya taarifa ya kusudio la kukata rufaa kutokuwa na sifa za kuwepo mahakamani. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Viongozi wa Chadema wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Freeman Mbowe walikata rufaa wakiiomba Mahakama Kuu iitishe jalada la kesi yao ya jinai kwa ajili ya kuchunguza na kujiridhisha kuhusu usahihi na uhalali wa mwenendo wa amri mbalimbali zilizotolewa na mahakama kuhusu kesi hiyo.

Hata hivyo, Mahakama hiyo imetupilia mbali rufaa hiyo kutokana na kuwepo kwa kasoro za kikanuni kwenye hati ya taarifa ya kusudio la kukata rufaa.

Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufaa, Eddy Fussi ndiye aliyesoma uamuzi huo leo tarehe 5 Oktoba 2018, ulioandaliwa na Jopo la Majaji wa Mahakama ya Rufaa waliosoma uamuzi huo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Jopo, Shaban Lila na Jacobs Mwambegele.

Kwa mujibu wa Naibu Msajili Fussi, taarifa ya kusudio la kukata rufaa haikubainisha kiini cha uamuzi na au amri ya Mahakama Kuu waliyokuwa wakiukatia rufaa.

Viongozi hao wa Chadema walikata rufaa wakipinga uamuzi wa Mahakama Kuu wa kutupilia mbali maombi ya mapitio ya mwenendo wa kesi yao ya msingi ya jinai, uliotolewa na Jaji Rehena Sameji katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

error: Content is protected !!