Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Mahakama Kuu yamtoa gerezani Lulu
MichezoTangulizi

Mahakama Kuu yamtoa gerezani Lulu

Elizabeth Michael 'Lulu'
Spread the love

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imembadilishia kifungo Msanii wa Filamu, Elizabeth Micheal ‘Lulu’ kutoka kwenye kifungo cha Magereza na kutumikia kifungo cha nje. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Lulu aliachiwa Mei 12 mwaka huu majira ya saa 2:30 asubuhi na kuanza kutumikia adhabu hiyo akiwa nje ya gereza.

Novemba 13 mwaka 2017 Lulu alihukumiwa kwenda jela miaka miwili baada ya kukutwa na hatia ya kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba bila kukusudia.

Hukumu hiyo ilitolewa na Jaji Sam Rumanyika baada ya kusikiliza ushahidi wa utetezi na ule wa Jamhuri.

Jeshi la Magereza limethibitisha kupokea amri ya mabadiliko adhabu ya msanii huyo ambapo atatolewa kutoka magereza na ataanza utaratibu wa adhabu ya kifungo cha nje.

Ofisa Habari wa Jeshi la Magereza, Lucas Mboje amesema Lulu amebadilishiwa adhabu na atatumikia kifungo cha nje kwa amri ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!