Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Mahakama Kenya yamkubali Kenyatta
Kimataifa

Mahakama Kenya yamkubali Kenyatta

Spread the love

MAHAKAMA ya Juu nchini Kenya imetupilia mbali kesi mbili zilizowasilishwa kupinga uchaguzi wa marudio, imeidhinishwa ushindi wa Kenyatta.

Jaji Mkuu David Maraga amesema majaji kwa kauli moja wameamua kwamba kesi zote mbili hazina msingi. Kesi ya Harun Mwau na wanaharakati wawili Njonjo Mue na Khelef Khalif zimetupiliwa mbali.

“Uchaguzi wa 26 Oktoba mwaka huu uliendeshwa sawa na na ushindi wa Kenyatta ni sahihi.
Kila upande utasimamia gharama yake,” amesema.

Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi wa urais wa marudio akiwa na kura 7,483,895 sawa na 98%.
Kiongozi wa upinzani Raila odinga aliyesusia uchaguzi huo alipata kura 73,228 sawa na asilimia 0.96.

Jumla ya wapiga kura 7,616,217 kati ya wapiga kura milioni 19.6 ambao walijiandikisha walishiriki uchaguzi huo.
Mahakama ya juu nchini humo ilifuta uchaguzi uliofanyika Septemba mwaka huu na kuamuru uchaguzi urudiwe ambao ulifanyika Oktoba 26 mwaka huu.

Katika uchaguzi uliofutwa na mahakama aliyekuwa mgombea urais kupitia Muungano wa NASA, Raila Odinga alipata kura zaidi ya milioni sita huku Kenyatta akiibuka na zaidi ya kura milioni nane.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Rais Tshisekedi amteua kiongozi wa wanamgambo kuwa Waziri wa Ulinzi

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi,...

Kimataifa

Raila Odinga: Tutafanya maandamano makubwa mara mbili kwa wiki

Spread the love KIONGOZI wa upinzani nchini Kenya, Raila Amollo Odinga ametangaza...

Kimataifa

Magharibi kuwekeza silaha Indo-Pacific, China yachochea

Spread the love KUVUNJIKA ushirhikiano wa China na Magharibi uliodumu kwa takribani...

Kimataifa

Ruto amlaumu Odinga kujaribu kuanzisha mgogoro kwa mara ya pili

Spread the love  RAIS wa Kenya William Ruto amesema kwamba hatakubali “kutoijali...

error: Content is protected !!