Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mahakama Kenya yamkubali Kenyatta
Kimataifa

Mahakama Kenya yamkubali Kenyatta

Spread the love

MAHAKAMA ya Juu nchini Kenya imetupilia mbali kesi mbili zilizowasilishwa kupinga uchaguzi wa marudio, imeidhinishwa ushindi wa Kenyatta.

Jaji Mkuu David Maraga amesema majaji kwa kauli moja wameamua kwamba kesi zote mbili hazina msingi. Kesi ya Harun Mwau na wanaharakati wawili Njonjo Mue na Khelef Khalif zimetupiliwa mbali.

“Uchaguzi wa 26 Oktoba mwaka huu uliendeshwa sawa na na ushindi wa Kenyatta ni sahihi.
Kila upande utasimamia gharama yake,” amesema.

Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi wa urais wa marudio akiwa na kura 7,483,895 sawa na 98%.
Kiongozi wa upinzani Raila odinga aliyesusia uchaguzi huo alipata kura 73,228 sawa na asilimia 0.96.

Jumla ya wapiga kura 7,616,217 kati ya wapiga kura milioni 19.6 ambao walijiandikisha walishiriki uchaguzi huo.
Mahakama ya juu nchini humo ilifuta uchaguzi uliofanyika Septemba mwaka huu na kuamuru uchaguzi urudiwe ambao ulifanyika Oktoba 26 mwaka huu.

Katika uchaguzi uliofutwa na mahakama aliyekuwa mgombea urais kupitia Muungano wa NASA, Raila Odinga alipata kura zaidi ya milioni sita huku Kenyatta akiibuka na zaidi ya kura milioni nane.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!