Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mahakama Afrika Kusini yataka Zuma arudishwe gerezani
Kimataifa

Mahakama Afrika Kusini yataka Zuma arudishwe gerezani

Jacob Zuma
Spread the love

 

Mahakama ya Afrika Kusini imeamua rais wa zamani wa Taifa hilo, Jacob Zuma anapaswa kurejea gerezani, kwa sababu msamaha wa kimatibabu aliopewa awali ulikuwa “kinyume cha sheria.” Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Muda aliokaa nje ya gereza haupaswi kuhesabiwa katika hukumu yake ya miezi 15, mahakama ya Pretoria ameamua.

Zuma aliachiliwa huru tarehe 5 Septemba 2021, kwa hali ya kiafya ambayo haikufichuliwa.

Alikuwa amefungwa gerezani kwa kushindwa kuhudhuria uchunguzi kuhusiana na na ufisadi wakati wa urais wake.

Zuma mwenye umri wa miaka 79 alijisalimisha kwa polisi Julai 2021, lakini kifungo chake, ambacho hakikutarajiwa kiliibua maandamano na uporaji, maeneo mbalimbali nchini humo.

Zaidi ya watu 300, wengi wao wakiwa ni kutoka katika ngome ya Zuma ya jimbo la KwaZulu-Natal, walifariki dunia katika maandamano hayo ya ghasia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!