Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo Maguire, Sterling waingia kikosi bora Euro, Ronaldo atupwa nje
Michezo

Maguire, Sterling waingia kikosi bora Euro, Ronaldo atupwa nje

Harry Maguire
Spread the love

NAHODHA wa Timu ya Taifa ya Uingereza Harry Maguire, Rahim Sterling na Kyle Walker wamejumuhishwa kwenye kikosi cha wachezaji 11 bora wa michuano ya Euro 2020. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea)

Michuano hiyo ambayo ilifikia ukingoni, tarehe 11 Julai 2021, kwa timu ya Taifa ya Italia kuibuka na ushindi wa penalti 3-2, dhidi ya Uingereza mara baada ya kumaliza dakika 90 kwa kufungana bao 1-1.

Mara baada ya michuano hiyo, Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA), imetoa majina 11 ya wachezaji wanaounda kikosi bora cha michuano hiyo na timu ya Taifa ya Italia ikiongoza kwa kutoa wachezaji watano.

Rahim Sterling

Katika kikosi hiko lilikosekana jina la mfungaji bora wa michuano hiyo Cristiano Ronaldo ambaye alicheza michezo minne na kupachika mabao 5.

Wengine waliochaguliwa kwenye kikosi hiko ni mchezaji bora wa michuano hiyo na mlinda mlango namba moja wa timu ya Taifa ya Italia, Donnarumma, Leornado Bonucci, Spinazolla.

Kwenye safu ya kiungo waliochaguliwa ni Jorginho, Pedro Gonzalez ‘Pedri’ na Pierre-Emile Hojbjerg, huku upande wa washambuliaji kukiwa na Romelu Lukaku pamoja na Federico Chiessa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!