Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli: Mkiniletea wale, hampati maji
Habari za Siasa

Magufuli: Mkiniletea wale, hampati maji

Spread the love

MGOMBEA urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli amesema, wananchi wa Tunduma, Mkoa wa Songwe wakichagua mgombea nje ya chama hicho, hatopeleka maji. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tunduma … (endelea).

Rais Magufuli amesema hayo leo Alhamisi tarehe 1 Oktoba 2020 wakati akihutubia mkutano wa kampeni zake za urais katika Viwanja vya Shule ya Sekondari ya Julius Kambarage Nyerere, Tunduma.

Amesema, sasa ni mara ya mwisho kuwaomba.
“…lakini msinichanganyie, mkiniletea hao nasema maji hamyapati. Lazima tuambizane ukweli na mimi nazungumzaga ukweli. Huwezi kupeleka chakula kwa jirani wakati mtoto wako ana njaa. Hata malaika wanachagua pa kwenda.”

“Huwezi watu unawabaembeleza kila siku. Miaka mitano iliyopita nilisimama kwenye uwanja nikawabembeleza, mkasema hapa na miaka mingine mkasema hapana. Hii ni mara ya mwisho mimi kuwaomba, siwatishi lakini ninasema ukweli,” amesema Dk. Magufuli.

David Silinde, mgonbea Ubunge jimbo la Tunduma kwa tiketi ya CCM

“Nimevumilia moyo mpaka unauma, mnataka niwaletee mpaka malaika? Hata Sodoma na Gomora Mungu alipowapelekea malaika, alivumilia mpaka akashindwa,” amesema

Dk. Magufuli amewataka wananchi wa jimbo hilo kumchagua David Silinde, mgombea ubunge wa kupitia CCM na kwamba, anamujua vizuri mgombea huyo na ndio maana alimpitisha kugombea ubunge licha kwamba kwenye kura za maoni hakuongoza.

“Mimi ni Mwenyekiti wa CCM, nisingempitisha huyu aliyekuwa Chadema, ninafahamu matunda yake na uzuri wake… hata CCM wapo waliokuwa wanampiga vita, hata Chadema alipotoka wapo wanaompiga vita.”

“Nileteeni Silinde halafu mje mniulize maji ya hapa…na ukweli nimeishaanza kuipanga hiyo miradi. Tunataka tuyatoe maji Ileje yateremke kwa mmiminika mpaka hapa Tunduma, mtakunywa mpaka mtachoka,” amesema.

Mgombea huyo amesema, kiasi cha Sh.2.579 bilioni zilitolewa kwa ajili ya miradi ya maji lakini mpaka sasa hakuna maji.

Amewataka wananchi wa jimbo hilo kumuuliza yule waliyemchagua kuhusu miradi ya maji kwa kuwa yeye hawezi kuwauliza.

“Ndio maana nasimama hapa kuwaomba ndugu zangu wa Tunduma, mniletee madiwani wa CCM, mniletee wabunge wa CCM ili kusudi pesa zitakapopotea, nijue namna ya kuwahoji, wale wengine siwezi kuwahoji, mkitakiwa nyinyi muwahoji. Sasa mniletee hawa ili niwahoji mmi mwenyewe,” amesema.

Frank Mwakajoka kutoka Chadema, ndiye aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo anayemaliza muda wake ambaye pia, anagombea tena jimbo hilo akichuana na Mwakajoka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!