Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli ateua mrithi wa aliyeshindwa kuapa
Habari za Siasa

Magufuli ateua mrithi wa aliyeshindwa kuapa

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Magufuli amemteua Profesa Shukrani Manya kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anaripoti Brightnes Boaz, Dar es Salaam … (endelea).

Pia, Profesa Manya ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Madini.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema, Profesa Manya ataapishwa leo Ijumaa mchana tarehe 11 Desemba 2020, Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

Kabla ya kiapo hicho cha uwaziri, saa 5:00 asubuhi ya leo, Spika wa Bunge, Job Ndugai atamwapisha kuwa Mbunge.

Kabla ya uteuzi huo, Profesa Manya alikuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Tanzania.

Profesa Manya, ameteuliwa kujaza nafasi ambayo Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Francis Ndulane alishindwa kuapa vizuri, kiapo cha naibu waziri.

Tukio hilo lilitokea Jumatano ya tarehe 9 Desemba 2020, Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma ambapo, Rais Magufuli aliwaapisha mawaziri 21 na naibu wao 22.

Rais Magufuli alisema, atafanya uteuzi wa naibu waziri mwingine wa madini ambaye ataweza kusoma vizuri nyaraka na Ndulane atasalia na nafasi yake ya ubunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

error: Content is protected !!