Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli amteua Dk. Bashiru kumrithi Balozi Kijazi
Habari za SiasaTangulizi

Magufuli amteua Dk. Bashiru kumrithi Balozi Kijazi

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Dk. Bashiru Ally kuwa Katibu Mkuu Kiongozi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaan … (endelea). 

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Bashiru alikuwa Katibu Mkuu wa chama tawala- Chama Chama Mapinduzi (CCM).

Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, leo Ijumaa usiku tarehe 26 Februari 2021, imesema, Dk. Bashiru, anachukua nafasi iliyoachwa na Balozi John Kijazi, aliyefariki dunia.

Balozi Kijazi, alifariki dunia tarehe 17 Februari 2021, katika Hospitali ya Benjamini Mkapa, Dodoma na mwili wake, kuzikwa nyumbani kwao, Korogwe mkoani Tanga.

Wakati huo huo, Msigwa amesema, Rais Magufuli amemteua Dk. Bashiru kuwa Balozi.

Uteuzi wa Dk. Bashiru unaanza leo na ataapishwa kesho Jumamosi saa 3:00 asubuhi Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!