Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli amteua Dk. Bashiru kumrithi Balozi Kijazi
Habari za SiasaTangulizi

Magufuli amteua Dk. Bashiru kumrithi Balozi Kijazi

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Dk. Bashiru Ally kuwa Katibu Mkuu Kiongozi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaan … (endelea). 

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Bashiru alikuwa Katibu Mkuu wa chama tawala- Chama Chama Mapinduzi (CCM).

Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, leo Ijumaa usiku tarehe 26 Februari 2021, imesema, Dk. Bashiru, anachukua nafasi iliyoachwa na Balozi John Kijazi, aliyefariki dunia.

Balozi Kijazi, alifariki dunia tarehe 17 Februari 2021, katika Hospitali ya Benjamini Mkapa, Dodoma na mwili wake, kuzikwa nyumbani kwao, Korogwe mkoani Tanga.

Wakati huo huo, Msigwa amesema, Rais Magufuli amemteua Dk. Bashiru kuwa Balozi.

Uteuzi wa Dk. Bashiru unaanza leo na ataapishwa kesho Jumamosi saa 3:00 asubuhi Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Askofu Bagonza: CDF Mabeyo amepasua masikio yetu

Spread the loveMJADALA kuhusu safari ya mwisho ya maisha ya Hayati Rais...

Habari za Siasa

10 matatani kwa kutorosha madini ya bil 1.5

Spread the loveJeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Kikosi...

Habari za Siasa

Wagombea 127 wa udiwani kutoka vyama 18 kuchaguliwa kesho

Spread the loveWagombea udiwani 127 kutoka vyama 18 vya siasa wanatarajiwa kupigiwa...

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

error: Content is protected !!