Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli amteua Dk. Bashiru kumrithi Balozi Kijazi
Habari za SiasaTangulizi

Magufuli amteua Dk. Bashiru kumrithi Balozi Kijazi

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Dk. Bashiru Ally kuwa Katibu Mkuu Kiongozi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaan … (endelea). 

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Bashiru alikuwa Katibu Mkuu wa chama tawala- Chama Chama Mapinduzi (CCM).

Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, leo Ijumaa usiku tarehe 26 Februari 2021, imesema, Dk. Bashiru, anachukua nafasi iliyoachwa na Balozi John Kijazi, aliyefariki dunia.

Balozi Kijazi, alifariki dunia tarehe 17 Februari 2021, katika Hospitali ya Benjamini Mkapa, Dodoma na mwili wake, kuzikwa nyumbani kwao, Korogwe mkoani Tanga.

Wakati huo huo, Msigwa amesema, Rais Magufuli amemteua Dk. Bashiru kuwa Balozi.

Uteuzi wa Dk. Bashiru unaanza leo na ataapishwa kesho Jumamosi saa 3:00 asubuhi Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!