Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Magufuli ampa kazi Dk. Shein, Mwakyembe
Habari Mchanganyiko

Magufuli ampa kazi Dk. Shein, Mwakyembe

Rais wa Tanzania, John Magufuli akiwa na Rais wa mstaafu wa Zanzibar Ali Mohamed Shein
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa viongozi watatu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu ya Tanzania, Gerson Msigwa imemnukuu, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi akiwataja walioteuliwa.

Kwanza, Rais Magufuli amemteua Rais mstaafu wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe.

Dk. Shein anachukua nafasi ya Jaji mstaafu Barnabas Samatta ambaye anamaliza muda wake.

Dk. Ali Mohamed Shein

Pili, Rais Magufuli amemteua Dk. Harrison Mwakyembe kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).

Dk. Mwakyembe aliyekuwa waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo, anachukua nafasi ya Mariam Joy Mwaffisi ambaye amemaliza muda wake.

Dk. Harisson Mwakyembe

Tatu, Rais Magufuli amemteua Gaudentia Kabaka kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Gaudensia ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), anashika wadhifa huo kwa kipindi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kumalizika.

Gaudensia Kabaka

Balozi Kijazi amesema, uteuzi wa viongozi hao umeanza leo Jumanne tarehe 24 Novemba, 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!