Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli ahofia kura za jazba
Habari za Siasa

Magufuli ahofia kura za jazba

Hayati John Magufuli, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM)
Spread the love

MGOMBEA urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Pombe Magufuli ameeleza kuhofia jazba katika upigaji kura kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 20202. Anaripoti Mwandishi Wetu, Bukoba … (endelea).

Akihutubia wananchi wa Kemondo-Bukoba Vijijini na Watanzania jana Jumanne tarehe 15 Septemba 2020 aliwaomba kumchagua ili aendelee kuiongoza Tanzania kwa miaka mitano mingine.

“Tusichague kwa jazba na kuangalia viongozi wapenda maneno, tukikosea tutajuta maana hakuna maendeleo mtakayoyaona,” amesema Dk. Magufuli.

Alisema, ingawa urais ni mateso, anaomba Watanzania wamruhusu kumaliza kipindi chake cha pili kisha apumzike.

Kauli ya kutoongeza dakika hata moja baada ya miaka mitano ijayo ya utawala wake, alikuwa akiirudia mara kwa mara.

“Naombeni mnipe miaka mitano tu, tutafanya makubwa katika muda huo, nikimaliza miaka yangu mitano hiyo, sitaki niongezewe hata siku moja, wapo wengine ndani ya CCM wanaoweza pia kuongoza, nataka nipumzike na mimi niangalie wengine wanavyofanya kazi,” alisema

“Sio kwamba napenda niwe rais, urais ni mateso, kazi yoyote ukitaka kuifanya vizuri ni mateso, nasema kwa dhati nikishamaliza miaka hii mitano sitaki kuongezewa hata siku moja.”

Akizungumzia mafanikio ndani ya miaka mitano ya utawala wake iliyopita, alisema Muleba imenufaika na zaidi ya Sh.65.32 bilioni zilizotolewa kwenye miradi ikiwemo ya afya, elimu, miundombinu na mingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

error: Content is protected !!