KAMPUNI ya New Habari 2006 LTD nchini Tanzania inayozalisha magazeti ya Dimba, Rai, Mtanzania na Bingwa imetangaza kusitisha uzalishaji wa magazeti yote kuanzia Jumatatu ijayo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Mhariri Mtendaji wa kampuni hiyo, Denis Msacky akizungumza na wafanyakazi leo Ijumaa tarehe 4 Desemba 2020 amesema, hatua hiyo inatokana na mwenendo wa biashara kuwa mbaya.
Msacky amesema, magazeti yote yataendelea kutoka hadi Jumatatu ya tarehe 7 Desemba 2020 yatakapositishwa rasmi.
Leave a comment