Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Magaidi wavamia, waua 49 msikitini New Zealand
Kimataifa

Magaidi wavamia, waua 49 msikitini New Zealand

Spread the love

HALI ya taharuki, wasiwasi na hofu imetanda kwa saa kadhaa katika mji wa Christchurch nchini New Zealand baada ya watu kadhaa kufanya shambulizi kubwa kwenye misikiti miwili na kuuawa watu 49 huku 48 wakijeruhiwa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Tukio hilo limetokea leo tarehe 15 Machi 2019 afajiri baada ya waumini wa Dini ya Kiislam kuhudhuria ibada ya alfajir kwenye msikiti wa Al Noor na Lin Wood iliyofikwa na mkasa huo.

Jacinda Arden, Waziri Mkuu wa New Zealand amezungumza na wanahabari katika mji mkuu wa nchi hiyo Wellington ambapo amesema, watu 10 waliofariki walishambuliwa katika msikiti wa kwanza wa Lin wood na 30 na baadaye watu tisa walipoteza maisha katika shambulio lililotekelezwa kwenye msikiti wa pili wa Al Noor.

Amesema, tukio hilo la kigaidi lilipangwa vilivyo na watuhumiwa kabla ya kutekelezwa akieleza kwamba, katika magari ya watuhumiwa kulikuwa na vifaa vya milipuko.

Arden amesema, tukio hilo linaashiria kwamba vitishio vya kiusalama katika taifa hilo vimeongezeka kutoka hali ya chini na kufikia kiwango cha juu.

Amewataka raia wa nchi hiyo kusikiliza ushauri wa polisi wa kwamba hali ya usalama iko vizuri.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi limewaweka kizuizini wanaume watatu na mwanamke mmoja wanaotuhumiwa kuhusika katika tukio hilo la kigaidi ambapo majeruhi wanapatiwa matibabu katika Hospitali ya Christchurch.

Scott Morrison, Waziri Mkuu wa Australia ameeleza kusikitishwa na hatua ya raia wa nchi yake kujihusisha na vitendo vya kigaidi jambo ambalo linachafua taswiraya nchi hiyo.

“Australia na New Zealand sio washirika tu, sisi ni wa familia moja. Leo tunahuzunika, tumeshtuka, tunashangaa na tumekasirishwa na tukio hilo,” amesema Morrison.

Baada ya kutokea tukio hilo Serikali ya Washngton imeeleza kuchukua tahadhari zaidi kulinda raia wake wa dini zote.

Polisi wa Los Angeles, New York na Minneapolis wameeleza kuwa wataimarisha zaidi ulinzi katika miji yote baada ya kutokea shambulizi nchini New Zealand.

“Hakuna tishio lolote kwa sasa hapa Marekani kwenye misikiti lakini tutaongeza ulinzi zaidi,” imeeleza taarifa ya polisi wa Minneapolis.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa, washambuliaji waliandika kurasa 87 na kuziweka kwenye mitandao ya kijamii wakieleza namna wanavyokerwa na wahamiaji wa Dini ya Kiislam nchini New Zealand.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!