Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Mafuriko yaua watu 29 Hebei China
Kimataifa

Mafuriko yaua watu 29 Hebei China

Spread the love

 

WATU 29 wamefariki na wengine 16 wamepotea kutokana na mafuriko yaliyotokea katika jimbo la Hebei nchini China. Imeripotiwa na Global Times … (endelea).

Mamlaka ya jimbo la Hebei imewaambia waandishi wa habari jana Ijumaa tarehe 11 Agosti 2023 kuwa imetenga kiasi cha Yuan 95.811 bilioni kwa ajili ya kujihami na maafa hayo.

Mamlaka hiyo imethibitisha vifo hivyo pamoja na kutoa rambirambi kwa familia zilizofiwa pamoja na kuwafariji wathirika wa mafuriko hayo.

Naibu Gavana wa Jimbo wa hilo Zheng Chengzhong amesema kuwa mafuriko hayo yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyoambatana na kimbunga.

Wizara ya Fedha pamoja na ile ya dharura nchini humo imeongeza pesa nyingine kiasi cha Yuan 1.46 bilioni kwa ajili ya kudhibiti maafa hayo.

Mpaka sasa serikali ishatumia kiasi cha Yuan 7.738 bilioni kwa ajili ya uokoaji katika majimbo matano ambayo ni Beijing, Tianjin, Hebei, Jilin na Heilongjiang.

Serikali ya China imetuma timu ya uokoaji katika maeneo yaliyoathiriwa kwa ajili ya kuwaokoa wananchi na imesema kuwa mpaka kufikia tarehe 1 Septemba wanafunzi wote watakuwa washarejea shuleni huku wananchi waliopoteza makazi wakipatiwa makazi mapya.

Watu 1.75 milioni wamehamishwa kwenye makazi yaliyoathiriwa ambapo tayari Serikali ishakarabati barabara 2237 zilizoharibika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

error: Content is protected !!