Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Maegesho Kayenzi na Kanyinya Kagera kujengwa
Habari Mchanganyiko

Maegesho Kayenzi na Kanyinya Kagera kujengwa

Mwita Waitara
Spread the love

 

WIZARA ya Ujenzi na Uchukuzi nchini Tanania, imetenga fedha kwa ajili ya kujenga maegesho ya Kayenzi na Kanyinya. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Jumanne, tarehe 18 Mei 2021, bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Ngara (CCM), mkoani Kagera, Ndaisaba Ruhoro.

“Je, ni lini serikali itapeleka Kivuko Mto Ruvuvu ili kuunganisha vijiji vya Mayenzi na Kanyinya vilivyoko wilaya ya Ngara,”ameuliza Ruhoro

Waitara amejibu, serikali imepanga kuendeleza kuboresha huduma za usafiri kwa njia ya maji, ikiwa ni pamoja na kuunganisha maeneo yenye mahitaji ya vivuko ikiwemo Kayenzi na Kanyinya kila inapopata fedha.

Amesema, aidha katika mwaka wa fedha 2021/22, serikali imetenga fedha kwa ajili ya kukamilisha maegesho hayo.

Mto Ruvuvu

“Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania(Temesa)uko kwenye hatua za ununuzi wa kumpata mkandarasi wa kufanya ujenzi wa maegesho ya kivuko
hicho.”

“Mkandarasi wa kufanya ukarabati wa kivuko kidogo, chenye uwezo wa kubeba abiria 60 na magari mawili ambacho hapo awali kilikuwa kinafanya kazi eneo la Rusomo-Nyakiziba(MV Ruvuvu ya zamani),”amesema Waitara.

Waitara amesema, baada ya ukarabati hupo kukamilika, kitatoa huduma kwenye eneo la kati ya Kayenzi hadi Kanyinya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!