Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Maegesho Kayenzi na Kanyinya Kagera kujengwa
Habari Mchanganyiko

Maegesho Kayenzi na Kanyinya Kagera kujengwa

Mwita Waitara
Spread the love

 

WIZARA ya Ujenzi na Uchukuzi nchini Tanania, imetenga fedha kwa ajili ya kujenga maegesho ya Kayenzi na Kanyinya. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Jumanne, tarehe 18 Mei 2021, bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Ngara (CCM), mkoani Kagera, Ndaisaba Ruhoro.

“Je, ni lini serikali itapeleka Kivuko Mto Ruvuvu ili kuunganisha vijiji vya Mayenzi na Kanyinya vilivyoko wilaya ya Ngara,”ameuliza Ruhoro

Waitara amejibu, serikali imepanga kuendeleza kuboresha huduma za usafiri kwa njia ya maji, ikiwa ni pamoja na kuunganisha maeneo yenye mahitaji ya vivuko ikiwemo Kayenzi na Kanyinya kila inapopata fedha.

Amesema, aidha katika mwaka wa fedha 2021/22, serikali imetenga fedha kwa ajili ya kukamilisha maegesho hayo.

Mto Ruvuvu

“Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania(Temesa)uko kwenye hatua za ununuzi wa kumpata mkandarasi wa kufanya ujenzi wa maegesho ya kivuko
hicho.”

“Mkandarasi wa kufanya ukarabati wa kivuko kidogo, chenye uwezo wa kubeba abiria 60 na magari mawili ambacho hapo awali kilikuwa kinafanya kazi eneo la Rusomo-Nyakiziba(MV Ruvuvu ya zamani),”amesema Waitara.

Waitara amesema, baada ya ukarabati hupo kukamilika, kitatoa huduma kwenye eneo la kati ya Kayenzi hadi Kanyinya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!