Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Maduka 400 kufungwa Arusha
Habari Mchanganyiko

Maduka 400 kufungwa Arusha

Spread the love

MADUKA zaidi ya 400 yako hatarini kufungwa na Halmashauri ya Jiji la Arusha, kutokana na wamiliki wake kushindwa kulipa malimbikizo ya kodi ya pango Sh. 262.5 milioni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Akizungumza na wanahabari jana tarehe 16 Aprili 2020, Anthony Kiwoli, Kaimu Mweka Hazina wa halmashauri hiyo, amesema maduka yatakayofungwa ni ya wafanyabiashara wenye madeni sugu, ambao hawajalipa kodi ya pango katika kipindi cha mwaka mmoja.

Kiwoli amewapa wafanyabaishara hao  siku 14 kulipa madeni yao, na kwamba agizo hilo lisipotekelezwa hadi kufikia Mei Mosi mwaka huu, maduka yao yatafungwa.

Amesema siku 14 zimetolewa baada ya viongozi wa wafanyabiashara hao, kuiomba Halmashauri ya Jiji la Arusha kuwapa muda wa kulipa deni hilo.

Maduka yanayotarajiwa kufungwa yako katika eneo la stendi ndogo jijini humo.

Akizungumzia agizo hilo, Loken Masawe, Mwenyekiti wa Wafanyabiashara mkoani Arusha, amesema kwa sasa anawahamasisha wafanyabiashara hao kulipa madeni yao katika kipindi walichopewa, ili maduka yao yasifungwe.

Masawe amesema wafanyabiashara hao walishindwa kulipa kodi hiyo kwa wakati husika kutokana na biashara kuwa ngumu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!