Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Maduka 400 kufungwa Arusha
Habari Mchanganyiko

Maduka 400 kufungwa Arusha

Spread the love

MADUKA zaidi ya 400 yako hatarini kufungwa na Halmashauri ya Jiji la Arusha, kutokana na wamiliki wake kushindwa kulipa malimbikizo ya kodi ya pango Sh. 262.5 milioni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Akizungumza na wanahabari jana tarehe 16 Aprili 2020, Anthony Kiwoli, Kaimu Mweka Hazina wa halmashauri hiyo, amesema maduka yatakayofungwa ni ya wafanyabiashara wenye madeni sugu, ambao hawajalipa kodi ya pango katika kipindi cha mwaka mmoja.

Kiwoli amewapa wafanyabaishara hao  siku 14 kulipa madeni yao, na kwamba agizo hilo lisipotekelezwa hadi kufikia Mei Mosi mwaka huu, maduka yao yatafungwa.

Amesema siku 14 zimetolewa baada ya viongozi wa wafanyabiashara hao, kuiomba Halmashauri ya Jiji la Arusha kuwapa muda wa kulipa deni hilo.

Maduka yanayotarajiwa kufungwa yako katika eneo la stendi ndogo jijini humo.

Akizungumzia agizo hilo, Loken Masawe, Mwenyekiti wa Wafanyabiashara mkoani Arusha, amesema kwa sasa anawahamasisha wafanyabiashara hao kulipa madeni yao katika kipindi walichopewa, ili maduka yao yasifungwe.

Masawe amesema wafanyabiashara hao walishindwa kulipa kodi hiyo kwa wakati husika kutokana na biashara kuwa ngumu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!