Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Madiwani wa CCM wamsusia Meya kikao
Habari za Siasa

Madiwani wa CCM wamsusia Meya kikao

Baraza la madiwani Manispaa ya Iringa wakiwa kikaoni
Spread the love

MADIWANI wa CCM katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wamegoma kushiriki kikao cha baraza la madiwani kilichotarajiwa kufanyika leo tarehe 7 Novemba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mkurugenzi wa Mansipaa ya Iringa Mjini ambaye ni Katibu wa kikao hicho, Hamid Njovu ameahirisha kikao hicho hadi tarehe 14 Novemba mwaka huu.

Madiwani wa Chadema ndio waliofika kwa ajili ya kushiriki kikao hicho, lakini idadi ya akidi haikutimia na kupelekea kikao hicho kutofanyika.

Kufuatia mgomo huo, Mwenyekiti wa CCM wilayani Iringa, Said Rubeya amesema madiwani wa CCM wako sahihi kutoshiriki kikao hicho, akisema kuwa meya wa manispaa hiyo, Alex Kimbe (Chadema) alikiuka kanuni.

Rubeya amedai kuwa, katika kikao cha CCM madiwani wa chama hicho walilalamikia ubabe wa meya huyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!