Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Madiwani Tanzania watangaziwa neema
Habari za Siasa

Madiwani Tanzania watangaziwa neema

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imependekeza kuanzia mwaka wa fedha 2021/22, itaanza kuwalipa madiwani posho za kila mwezi kutoka serikali kuu. Anaripoti Jemima Samwel, DMC…(endelea).

Hayo yamesemwa leo Alhamisi, tarehe 10 Juni 2021 na Dk. Mwigulu Nchemba, alipokuwa anawasilisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2021/22, bungeni jijini Dodoma.

Amesema, madiwani wenzetu wanafanya kazi nzuri sana za kusimamia shughuli za maendeleo kwenye kata zetu.

“Hawa ni wabunge wakaazi wa kwenye kata zetu ambao kila siku wako na wananchi wetu kwenye kusimamia shughuli za maendeleo.”

“Hata hivyo, katika baadhi ya halmashauri madiwani wamekuwa wakikopwa posho zao, na wengine hufikia hatua ya kupiga magoti kwa wakurugenzi watendaji ili walipwe,” amesema

Amesema, hali hii imekuwa ikipunguza ufanisi katika halmashauri zetu kwa madiwani wengi kufanya maamuzi yanayopendekezwa na wakurugenzi watendaji hata kama hayana maslahi kwa Taifa ili waweze kulipwa posho zao.

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango

Waziri huyo amesema, jambo hilo limeongelewa kwa hisia kali sana na waheshimiwa wabunge hapa bungeni.

“Waheshimiwa Wabunge na Waheshimiwa Madiwani, napenda niwaeleze kuwa Mama yetu amesikia kilio chenu na alinielekeza mimi pamoja na Waziri wa TAMISEMI kulitafutia ufumbuzi suala hili,” amesema

Huku wabunge wakishangilia, Dk. Mwigulu amesema “napendekeza kuanzia mwaka 2021/22, Serikali Kuu ianze kulipa posho za kila mwezi za Madiwani moja kwa moja tena kwenye akaunti zao kwa Halmashauri zote zenye uwezo mdogo kimapato.”

Kuhusu halmashauri 16 zenye uwezo mkubwa wa kimapato (Daraja A) , Dk. Mwigulu amesema “zitaendelea kutumia mapato yake ya ndani kulipa posho za Madiwani kupitia kwenye akaunti zao.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!