Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Madini ya Tanzanite: Rais Samia ampa maagizo Biteko
Habari za SiasaTangulizi

Madini ya Tanzanite: Rais Samia ampa maagizo Biteko

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemwagiza Waziri wa Madini, Doto Biteko kukaa na wawekezaji ili kuangalia njia bora ya kuyalinda madini ya Tanzanite yanayopatikana nchini humo pekee dunia nzima. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Samia ametoa agizo hilo leo Jumapili, tarehe 13 Juni 2021, katika siku ya kwanza kati ya tatu ya ziara yake mkoani Mwanza, alipokuwa akifungua Kiwanda cha Kusafisha Dhahabu.

“Nimeingia ndani nimeoneshwa kiwanda cha kusafisha dhahabu-Mwanza kinavyofanya kazi, kwa maneno mengine ni miujizi, nimeonyeshwa unavyofanya kazi ni dakika tatu,” amesema.

Katika maelezo yake, Rais Samia amesema, “tudhibiti wizi na utoroshaji wa magendo ya madini yetu hususan kwenye migodi yetu ya dhababu na waziri (Biteko), kwenye mgodi wa Tanzanite.”

“Mungu aliipendelea Tanzania pekee akaipa Tanzanite, lakini tunavyokwenda sasa hivi, ni kama inachimbwa dunia nzima, ukienda kwa majirani zetu, Asia yapo. Nimesema, rasilimali zetu, zinakwenda na kumalizika kwa hiyo Tanzanite yetu inaweza kumalizika,” amesema.

Rais Samia amesema, “kuna haja ya kuwa na shirika la kudhibiti Tanzanite yetu, kuwa Tanzanite yote iliyoko mkononi imilikiwe na huyu, nikuombe sana Waziri, kaa na wawekezaji kwenye sekta hii ili kuona jinsi ya kuilinda Tanzanite yetu.”

Waziri wa Madini, Doto Biteko

Pia, Rais Samia maagizo kwa wizara ya madini kuhakikisha “inafuatilia watu waliochukua maeneo lakini hawayaendelezi, ule mtindo wa tajiri mmoja kuchukua maeneo lakini hayaendelezi, naomba liishie hapa.”

Awali, Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila alisema, kiwanda hicho, kilichozinduliwa kilianza kujengwa 15 Machi 2020 na kukamilika Machi 2021, kikiwa kimegharimu Sh.12 bilioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!