Wednesday , 27 September 2023
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Machafuko yaibuka Kenya, watano wapigwa risasi
Makala & Uchambuzi

Machafuko yaibuka Kenya, watano wapigwa risasi

Mkuu wa Polisi katika mji wa Nairobi, Japheth Koome
Spread the love

WATU 5 wamepigwa risasi katika ghasia zilizotokea nchini Kenya baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika juzi nchini Kenya, anaandika Hellen Sisya.

Ghasia hizo zimetokea jana baada ya kinara wa kambi ya upinzani, Raila Odinga kudai kuwa kumefanyika udanganyifu mkubwa.

Mkuu wa Polisi katika mji wa Nairobi, Japheth Koome amesema watu wawili waliuawa kwa kupigwa risasi jana akisisitiza kuwa walitumia machafuko kupora mali za watu.

Mtu mwingine aliuawa mapema jana kwa kupigwa risasi na polisi katika kaunti ya Kisii nje ya Shule ya Sekondari ya Nduru ambayo ilikuwa na kituo cha kuhesabu kura za uchaguzi wa rais katika jimbo la uchaguzi la Mugirango.

Katika mji wa Kisumu ambao ndiyo ngome kuu ya kinara wa upinzani Raila Odinga, polisi ilitumia gesi ya kutoa machozi na risasi kutawanya waandamanaji waliokuwa wakipinga matokeo ya uchaguzi wa rais.

Matokeo ya awali yaliyotolewa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya (IEBC) yanaonesha kuwa, mgombea wa chama cha Jubilee, Uhuru Kenyatta anaongoza kwa kura milioni 7.9 sawa na asilimia 53.89 ya kura zilizohesabiwa huku mpinzani wake mkuu, Raila Odinga akiwa na kura 6.5 sawa na asilimia 44.47 ya kura.

Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani cha NASA, Raila Odinga amepinga matokeo hayo akisema yamechakachuliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Prof Mwafenga ulijiamini katika utendaji wako na degree zako 10 – Maige

Spread the loveKIFO cha Prof Hadley Mpoki Mwafenga- Afisa Usimamizi wa Fedha...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Hii ndio sura halisi ya Rais Samia

Spread the loveKILA zama na kitabu chake. Hizi ni zama za Rais...

Makala & Uchambuzi

Safari ya Siah Malle katika uhandisi inavyoibua vipaji vipya vya wanawake

Spread the loveSiah Malle ni mfano mzuri wa mwanamke ambaye amefanikiwa kuvunja...

Makala & Uchambuzi

Rekodi ya watalii kuandikwa Desemba 2023

Spread the love  WIZARA ya Maliasili na Utalii imesema ifikapo Desemba 2023...

error: Content is protected !!