Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Machafuko yaibuka Kenya, watano wapigwa risasi
Makala & Uchambuzi

Machafuko yaibuka Kenya, watano wapigwa risasi

Mkuu wa Polisi katika mji wa Nairobi, Japheth Koome
Spread the love

WATU 5 wamepigwa risasi katika ghasia zilizotokea nchini Kenya baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika juzi nchini Kenya, anaandika Hellen Sisya.

Ghasia hizo zimetokea jana baada ya kinara wa kambi ya upinzani, Raila Odinga kudai kuwa kumefanyika udanganyifu mkubwa.

Mkuu wa Polisi katika mji wa Nairobi, Japheth Koome amesema watu wawili waliuawa kwa kupigwa risasi jana akisisitiza kuwa walitumia machafuko kupora mali za watu.

Mtu mwingine aliuawa mapema jana kwa kupigwa risasi na polisi katika kaunti ya Kisii nje ya Shule ya Sekondari ya Nduru ambayo ilikuwa na kituo cha kuhesabu kura za uchaguzi wa rais katika jimbo la uchaguzi la Mugirango.

Katika mji wa Kisumu ambao ndiyo ngome kuu ya kinara wa upinzani Raila Odinga, polisi ilitumia gesi ya kutoa machozi na risasi kutawanya waandamanaji waliokuwa wakipinga matokeo ya uchaguzi wa rais.

Matokeo ya awali yaliyotolewa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya (IEBC) yanaonesha kuwa, mgombea wa chama cha Jubilee, Uhuru Kenyatta anaongoza kwa kura milioni 7.9 sawa na asilimia 53.89 ya kura zilizohesabiwa huku mpinzani wake mkuu, Raila Odinga akiwa na kura 6.5 sawa na asilimia 44.47 ya kura.

Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani cha NASA, Raila Odinga amepinga matokeo hayo akisema yamechakachuliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMakala & Uchambuzi

Kanda ya Ziwa yaonyesha NMB inavyosaidia afya ya mama na mtoto

Spread the loveMafanikio inayozidi kupata Tanzania katika kupunguza vifo vya mama na...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

‘Mwanapekee’ wa Rais Samia: Atabadili nini Arusha?

Spread the loveMAPEMA wiki hii, baadhi ya viongozi walioapishwa na Rais Samia...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kipunguni waihoji serikali, ziko wapi fedha za fidia?

Spread the loveWATU wanaodai kwamba serikali ya Chama Cha Mapinduzi ni sikivu,...

Habari za SiasaMakala & UchambuziTangulizi

Askofu Bagonza: Tusichonganishwe; tusichokozane na tusikufuru

Spread the loveJOTO la chaguzi linapanda kila siku hapa nchini. Upo umuhimu...

error: Content is protected !!