Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mabasi ya masafa marefu sasa lazima kuwa na madereva wawili
Habari Mchanganyiko

Mabasi ya masafa marefu sasa lazima kuwa na madereva wawili

Mabasi yakiwa kituo cha mabasi Mbezi
Spread the love

 

WAZIRI Mkuu nchini Tanzania, Kassim Majaliwa, ameliagiza Jeshi la Polisi nchini humo kuhakikisha wanakagua mabasi yote ya masafa marefu na kujiridhisha kuwa yana madereva wawili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza…(endelea).

Majaliwa ametoa agizo hilo leo Jumanne tarehe 14 Machi, 2023 wakati akizindua Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani inayofanyika kitaifa mkoani Mwanza.

Majaliwa amesema uchunguzi unaonesha kuwa mabasi hususani yanayoenda mikoani na safari ndefu, ni miongoni mwa wahanga wakubwa wa ajali za barabarani kwasababu yakutofuata kanuni.

Amesema taratibu zilizowekwa na usalama barabarani ni mabasi hayo kuwa na madereva wawili ili kupokezana.

“Kumpa dereva mmoja aendeshe kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza huo ni uzembe na hivyo basi nilielekeze jeshi la polisi na wasimamizi wengine wa sheria haya makampuni yanayokwenda umbali mrefu lazima yawahakikishie kuwa yana dereva zaidi ya mmoja ambao wataendesha kuelekea huko wanakokwenda kwa safari ndefu,” amesema Majaliwa.

Aidha amewataka wamiliki wa mabasi nao wahakikishe basi la mbali mrefu linakuwa na dereva zaidi ya mmoja.

“Serikali kwa upande wetu tutaendelea kuboresha miondombinu lengo hapa ni kukuza shughuli za usafirishaji ziwe nzuri Zaidi, mnaonunua magari yaendelee kuwa na hali nzuri,” amesema.

Majaliwa ametaja sababu zinazosababisha ajali kuwa ni pamoja ni watu kuendesha bila kuwa na mafunzo wala leseni ya kuendesha vyombo vya moto, kubeba abiria zaidi ya mmoja kwenye pikipiki, kutumia vilevi na kuendesha vyombo vya moto, kutumia simu, kuzidisha mizigo au abiria zaidi ya uwezo wa chombo chenyewe.

Amesema hivi sasa jeshi la polisi linakwenda kuimarisha usimamizi kuanzia kwenye vyuo vya kujifunza udereva, “kwahiyo kila mkoa najua vyuo hivyo vipo endeleeni kukaa pamoja na jeshi la polisi na hakikisheni mnatengeneza madereva wazuri.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!