Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Mabasi ya masafa marefu sasa lazima kuwa na madereva wawili
Habari Mchanganyiko

Mabasi ya masafa marefu sasa lazima kuwa na madereva wawili

Mabasi yakiwa kituo cha mabasi Mbezi
Spread the love

 

WAZIRI Mkuu nchini Tanzania, Kassim Majaliwa, ameliagiza Jeshi la Polisi nchini humo kuhakikisha wanakagua mabasi yote ya masafa marefu na kujiridhisha kuwa yana madereva wawili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza…(endelea).

Majaliwa ametoa agizo hilo leo Jumanne tarehe 14 Machi, 2023 wakati akizindua Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani inayofanyika kitaifa mkoani Mwanza.

Majaliwa amesema uchunguzi unaonesha kuwa mabasi hususani yanayoenda mikoani na safari ndefu, ni miongoni mwa wahanga wakubwa wa ajali za barabarani kwasababu yakutofuata kanuni.

Amesema taratibu zilizowekwa na usalama barabarani ni mabasi hayo kuwa na madereva wawili ili kupokezana.

“Kumpa dereva mmoja aendeshe kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza huo ni uzembe na hivyo basi nilielekeze jeshi la polisi na wasimamizi wengine wa sheria haya makampuni yanayokwenda umbali mrefu lazima yawahakikishie kuwa yana dereva zaidi ya mmoja ambao wataendesha kuelekea huko wanakokwenda kwa safari ndefu,” amesema Majaliwa.

Aidha amewataka wamiliki wa mabasi nao wahakikishe basi la mbali mrefu linakuwa na dereva zaidi ya mmoja.

“Serikali kwa upande wetu tutaendelea kuboresha miondombinu lengo hapa ni kukuza shughuli za usafirishaji ziwe nzuri Zaidi, mnaonunua magari yaendelee kuwa na hali nzuri,” amesema.

Majaliwa ametaja sababu zinazosababisha ajali kuwa ni pamoja ni watu kuendesha bila kuwa na mafunzo wala leseni ya kuendesha vyombo vya moto, kubeba abiria zaidi ya mmoja kwenye pikipiki, kutumia vilevi na kuendesha vyombo vya moto, kutumia simu, kuzidisha mizigo au abiria zaidi ya uwezo wa chombo chenyewe.

Amesema hivi sasa jeshi la polisi linakwenda kuimarisha usimamizi kuanzia kwenye vyuo vya kujifunza udereva, “kwahiyo kila mkoa najua vyuo hivyo vipo endeleeni kukaa pamoja na jeshi la polisi na hakikisheni mnatengeneza madereva wazuri.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yakabidhi rasmi msaada nchini Malawi

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Bashe: Tumeshagawa pikipiki 5,500 kati ya 7,000 kwa maafisa ugani

Spread the love  WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amesema wizara hiyo tayari...

Habari Mchanganyiko

Spika Tulia awapa neno mawaziri utekelezaji mashamba ya pamoja

Spread the love  SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amewataka mawaziri kushirikiana...

Habari Mchanganyiko

Ukosefu wa maadili kwa wakunga, wauguzi bado changamoto

Spread the loveIMEELEZWA kuwa vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa  wauguzi na...

error: Content is protected !!