Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mabasi 165 ya mwendokasi kuongezwa Dar
Habari za Siasa

Mabasi 165 ya mwendokasi kuongezwa Dar

Mabasi ya Mwendokasi
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imesema mchakato unafanyika kununua mabasi 165 ili kupunguza adha ya usafiri wa mradi wa mabasi yaendayo haraka katika Jiji la Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea)

Hayo yamesemwa leo Jumatano tarehe 13 Mei 2020 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) wakati akijibu swali la Aysharose Mattembe, Mbunge wa Viti Maalumu kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).

Aysharose amesema uamuzi wa Serikali kutengeneza miundombinu ya usafiri wa Mabasi ya Mwendokasi ulilenga kuondoa kero kwa wananchi jijini Dar es Salaam, lakini usafiri huu umekuwa kero kubwa kwa watumiaji ikiwemo kujaza abiria bila kujari athari za watumiaji.

“Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti ujazaji abiria pamoja na kuweka utaratibu mzuri kwa watumiaji wake,” ameuliza

Akijibu swali hilo, Waziri wa Tamisemi amesema, ili kupunguza msongamano wa abiria, Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka jijini Dar es Salaam (DART) unaendelea na taratibu za ununuzi ili kumpata mzabuni atakayeongeza idadi ya mabasi kutoka 140 yaliyopo sasa hadi 305.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!