Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mabadiliko ya tabia nchi yaua mifugo, wanyamapori 38,720 Longido
Habari Mchanganyiko

Mabadiliko ya tabia nchi yaua mifugo, wanyamapori 38,720 Longido

Mkurugenzi wa Shirika la MAIPAC Mussa Juma akizungumza mbele ya washiriki wa mkutano huo.
Spread the love

 

MABADILIKO ya tabia nchi, yameua mifugo na wanyamapori zaidi ya 38,720 kwa kukosa maji na malisho, wilaya ya Longido mkoa wa Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha… (endelea).

Afisa Mifugo na Mabadiliko ya tabia nchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Nestory Daqarro alitoa taarifa hiyo jana tarehe 17 Oktoba, 2022 katika mkutano wa uhakiki wa taarifa.

Mkutano huo ulioandaliwa na taasisi ya wanahabari ya usaidizi wa jamii za pembezoni( Media Aid For Indigenous and Pastoralist Community-MAIPAC) kwa udhamini wa shirika la maendeleo la umoja wa mataifa(UNDP) kupitia mfuko wa mazingira Duniani(GEF) na kuratibiwa na jumuiko la maliasili Tanzania(TNRF).

Mkutano huo ulilenga kujadili umuhimu maarifa ya asili katika utunzwaji vyanzo vya maji, misitu na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Daqaro alisema katika kipindi cha miezi tisa,wanyama takribani 38,720 wamekufa wakiwepo Twiga wanne, Pundamilia 18,Swala 2 na wengine ni Ng’ombe, kondoo na mbuzi .

“Jitihada zinaendelea kufanywa hapa wilayani ikiwepo kuchimba visima na kupeleka maji maeneo ya wanyama, kutenga malisho ili kuokoa maisha ya wanyama na uchumi wa wilaya hiyo, ambapo asilimia 95 ya wananchi hutegemea mifugo”alisema

Mkurugenzi wa jumuiko la Maliasili Tanzania(TNRF), Zakaria Faustine, alisema kuna haja kuwa na mkakati shirikishi baina ya asasi za kiraia, serikali, mashirika ya kimataifa na wananchi kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Mkurugenzi wa Shirika la CILAO, Odero Odero akizungumza mbele ya wadau

Faustine alisema mradi wa kukusanya maarifa ya asili yanayoweza kutumika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, kutunza misitu na maji ambao unatekelezwa na MAIPAC ni sehemu ya mkakati wa kupata taarifa ili kusaidia maboresho ya sera na sheria nchini.

“Tunawapongeza MAIPAC na CILAO kwa mradi huu, ambao unatekelezwa pamoja na miradi mingine 12 ya mazingira ambayo inafadhiliwa na UNDP kupitia programu ya miradi midogomidogo kwa lengo na kushirikisha jamii za asili katika utunzwaji wa mazingira na vyanzo vya maji”alisema

Mwenyekiti wa kijiji cha Kimokowa, wilaya ya Longido, Kilei Mollel alisema licha ya wilaya hiyo, kukabiliana na ukame na kukosa maji pia imeibuka mimea vamizi ambayo hailiwi na mifugo na wanyamapori ambayo imeota katika maeneo mengi.

“Tumekuwa tukishirikiana na serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali kama CORDs kung’oa mimea lakini ni mingi zaidi ya hekali 1000 za malisho zimevamiwa”alisema.

Mkurugenzi MAIPAC, Mussa Juma na Mkurugenzi wa shirika la CILAO, Odero Odero walieleza katika mradi huo wamefika katika wilaya tatu za Monduli, Longido na Ngorongoro na kukutana na makundi ya wazee maarufu, viongozi wa mila, wanawake, vijana na wanafunzi na kukusanya maarifa za asili katika masuala ya mazingira.

Juma alisema jamii za pembezoni zina utajiri mkubwa wa maarifa ya asili lakini, kama yasipohifadhiwa yanaendelea kutoweka na hivyo, jamii kutegemea elimu za kisasa pekee katika utunzwaji wa mazingira.

Kwa upande wake Odero alifafanua kuwa, maarifa ya asili ambayo yatakusanywa katika mradi huo, yatawekwa katika vitabu na kwenye vyombo vya habari ili kuzalia kutumika katika utungaji wa sera lakini pia kuelimisha jamii umuhimu wa maarifa hayo.

Wadau wakiwa katika picha ya pamoja kujadili madhara ya mabadiliko ya tabianchi katika Wilaya ya Longido mkoani Arusha

Afisa misitu wa tarafa ya Makuyuni na Manyara, Hapiness Masaki na Afisa misitu wa Wakala wa misitu(TFS) wilaya ya Ngorongoro, Major Ngoilenya walisema ni muhimu maarifa ya asili kutumika katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi katika kutunza vyanzo vya maji na misitu.

Mkurugenzi wa shirika la MIMUTIE women Orgganization (MWO) Rose Njilo akizungumza katika mkutano huo, licha ya kupongeza mradi wa kukusanya taarifa za maarifa ya asili unaotekelezwa na shirika la MAIPAC, alisema hivi sasa wanaoathirika na mabadiliko ya tabia nchi ni wanawake na watoto.

“Mradi huu umekuja wakati muafaka sasa elimu ya asili itambulike na watunga sera ili iweze kuwasaidia wanawake na watoto jamii za pembezoni ambao ndio waathirika wakubwa wa mabadiliko ya tabia nchi”alisema.

Afisa habari wa shirika la PINGOs Forums, Elie Chansa alitaka taarifa za asili ambazo zitakusanywa katika mradi huo,zifikishwe serikalini na katika mashule na vyuo ili ziweze kutumika katika kutunza mazingira kabla walivyofanya mababu.

Mradi wa kukusanya taarifa za uhifadhi mazingira, kutunza vyanzo vya maji, misitu na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, unatekelezwa na shirika la MAIPAC kwa kushirikiana na shirika la CILAO katika wilaya tatu za mkoa Arusha ambazo ni Longido, Monduli na Ngorongoro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!