Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Maandamano Sudan yamng’oa waziri mkuu aliyewekwa na jeshi
Kimataifa

Maandamano Sudan yamng’oa waziri mkuu aliyewekwa na jeshi

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Sudan, Abdalla Hamdok, aliyewekwa madarakani na jeshi la nchi hiyo Novemba 2021, amejiuzulu kufuatia maandamano ya wananchi, wanaoshinikiza utawala kisiasa na kiraia. Unaripoti Mtandao wa BBC Swahili … (endelea).

Hamdok alitangaza hatua hiyo jana Jumapili, tarehe 2 Januari 2022, baada ya  kuibuka maandamano ya wananchi wanaopinga makubaliano kati ya Waziri Mkuu huyo na Jeshi la Sudan. Watu wawili wamepoteza maisha katika maandamano hayo.

Akihutubia wananchi  kupitia Televisheni ya Taifa ya Sudan, Hamdok alisema amejiuzulu, ili kuinusuru nchi hiyo iliyokuwa katika kipindi cha hatari kinachotishia ustawi wake.

“Niliamua kurudisha jukumu hilo na kutangaza kujiuzulu uwaziri mkuu, na kutoa nafasi kwa mwanaume au mwanamke mwingine wa nchi hii adhimu, ili kuisaidia kupita kile kilichosalia cha kipindi cha mpito kwa nchi kuelekea utawala wa kidemokrasia ya kiraia,” alisema Hamdok.

Wananchi wa Sudan wanapinga makubaliano ya Jeshi la nchi hiyo na Hamdok, ya kugawana madaraka na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan,  kiongozi wa mapinduzi yaliyonng’oa madarakani aliyekuwa Rais wao,  Omar al Bashir.

al Bashir aling’olewa madarakani  kwa mapinduzi ya kijeshi 2019, kisha Serikali ya Mpito iliundwa na Jeshi, iliyodumu kwa muda mfupi baada ya wananchi kuandamana wakishinikiza upatikanaji wa Serikali ya kidemokrasia.

Kufuatia maandamano hayo,  Hamdok aliwekwa madarakani kwa ajili ya kuongoza Serikali ya mpito hadi 2023, Taifa hilo litakapofanya uchaguzi wa kuunda Serikali ya kiraia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!