Friday , 9 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Maandamano Kenya, Afrika Kusini yashika kasi, wapinzani wakishikiliwa
Kimataifa

Maandamano Kenya, Afrika Kusini yashika kasi, wapinzani wakishikiliwa

Spread the love

 

MAANDAMANO ya kupinga serikali zilizoko madarakani nchini Kenya na Afrika Kusini, yameendelea kushika kasi katika mataifa hayo, huku baadhi ya walioandamana wakitiwa nguvuni na Jeshi la Polisi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Maandamano nchini Kenya yaliitishwa na aliyekuwa Mgombea Urais wa Kenya kupitia Chama cha Azimio la Umoja, Raila Odinga, huku ya nchini Afrika Kusini, yakiitishwa na chama cha upinzani cha Economic Freedom Fighters, ambayo yanafanyika leo Jumatatu,tarehe 20 Machi 2023.

Huko nchini Kenya, Jeshi la Polisi linajaribu kuyazuia maandamano yanayofanyika jijini Nairobi ambapo waandamanaji wanalenga kutinga Ikulu ya taifa hilo, ambapo hadi sasa wabunge wa upinzani, Amina Mnyazi na Ken Chonga, pamoja na seneta wa Kilifi, Stewart Madzayo, wamekamatwa.

Pia, aliyekuwa Spika wa Kaunti ya Nakuru na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha ODM, katika kaunti hiyo, Joel Kairu, amekamatwa na Jeshi la Polisi.

Licha ya wapinzani hao kukamatwa, Azimio la Umoja kupitia akaunti yake ya Twitter, umeandika ukisema hautarudi nyuma katika maandamano hayo.

Wakati wabunge hao wa Kenya wakitiwa nguvuni, nchini Afrika Kusini watu takribani 100 walioshiriki maandamano wameripotiwa kukamatwa na Jeshi la Polisi kwa madai kwamba wamefanya maandamano ya fujo.

Waziri wa Polisi nchini humo, Bheki Cele, ametoa taarifa akisema asilimia kubwa ya waliokamatwa wanatoka Jimbo la Gauteng.

Cele amedai kuwa, waliokamatwa walikuwa wakitengeneza vilipuzi vya moto, kufunga barabara na kujaribu kuwazuia watu kwenda kazini.

Maandamano hayo ya nchini Afrika Kusini,yanalenga kumshinikiza Rais wa taifa hilo, Cyril Ramaphosa ajiuzulu kwa madai kuwa ameshindwa kutekeleza majukumu yake katika kuimarisha uchumi, kuongeza ajira na kupunguza makali ya ugumu wa maisha.

Nako nchini Kenya, maandamano yanalenga kumshinikiza Rais William Ruto, ajiuzulu kwa madai kwamba ameshindwa kudhibiti mfumuko wa bei.

8 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Kagame afumua tena Jeshi, awafuta kazi maofisa zaidi ya 200 wakiwemo majenerali

Spread the love  RAIS wa Rwanda, Paul Kagame, amewafuta kazi Meja Jenerali...

Kimataifa

Urusi imelipua bwawa kuu la umeme nchini Ukraine

Spread the loveSERIKALI mjini Kyiv nchini, Ukraine imeushutumu utawala wa Rais Vladimir...

Kimataifa

Rais Kagame afanyia mabadiliko makubwa jeshi, usalama wa taifa

Spread the loveRAIS wa Rwanda, Paul Kagame amefanye uteuzi wa wakuu wapya...

Kimataifa

Miili ya waliofariki kwenye ajali ya treni India, kukabidhiwa baada ya vipimo vya DNA

Spread the love  TAKRIBANI watu 260 wamefariki na wengine karibu 650 wamejeruhiwa...

error: Content is protected !!