Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Maambukizi ya VVU yapiga kambi kwa wanandoa
Habari Mchanganyiko

Maambukizi ya VVU yapiga kambi kwa wanandoa

Spread the love

WATU waliofunga ndoa na kuunganika kuwa kama mwili mmoja na kuepukana na masuala ya kufanya ngono zembe, imebainishwa wao kwa sasa ndio wamekuwa vinara wa kupata maambukizi mapya ya Virusi Vya Ukimwi (VVU), kutokana na kutozingatia sheria na kanuni za ndoa, ananadika Mwandishi Wetu.

Imeelezwa kuwa watu wamekuwa wakiingia kwenye ndoa kama fasheni, bila ya kufahamu nini maana ya kufunga pingu hizo za maisha, na kujikuta baada ya muda mfupi wamechokana na kuanza kufarakana.

Hayo yalizungumzwa juzi na mwandishi wa kitabu cha Sakramenti ya ndoa katika nyumba aminifu Paschal Maziku, wakati akikitambulisha kwa waumini wa Kanisa Katoliki mjini Shinyanga.

“Tulifanya utafiti na kugundua wanandoa ndio wamekuwa vinara wa maambukizi mapya ya VVU, ambapo kisheria wanandoa ndio wanapaswa kuwa salama sababu kabla ya kufunga pingu za maisha huwa wanapimwa afya zao, lakini kwa hali ya sasa imebadilika na wengi wao ndio
waathirika wa Ukimwi,” amesema Maziku

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!