Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Maambukizi ya UVIKO-19 yaongezeka
Afya

Maambukizi ya UVIKO-19 yaongezeka

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imesema maambukizi ya ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO-19), katika kipindi cha tarehe 29 Oktoba hadi 2 Desemba 2022, yameongezeka kwa asilimia 62.5, kutoka visa vipya 272 hadi kufikia 442. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana Jumatatu, tarehe 6 Desemba 2022 na Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Tumaini Nagu, akitoa mwenendo wa UVIKO-19 nchini.

“Serikali imeendelea kuimarisha mapambano dhidi ya UVIKO-19 nchini na inaendelea kutoa taarifa kwa umma kuhusu mwenendo wa ugonjwa huu. Katika kipindi cha tarehe 29 Oktoba hadi 2 Desemba 2022, jumla ya visa vipya 442 vimethibitika kuwa na maambukizi ya UVIKO-19. Idadi hii ni kubwa ukilinganisha na takwimu za mwezi ulipita ambapo kulikuwa na visa 272 sawa na ongezeko la asilimia 62.5,” imesema taarifa ya Prof. Nagu.

Aidha, taarifa ya Prof. Nagu imesema hakuna mgonjwa aliyelazwa wala kifo kutokana na ugonjwa huo ulioibuka 2019.

Taarifa ya Prof. Nagu imesema hadi kufikia tarehe 2 Desemba 2022, watu 29,123,387 kati ya walengwa 30,740,928 ambao ni sawa na asilimia 94.7 wamepata dozi kamili ya chanjo ya UVIKO-19, ili kuwawezesha wananchi kupata kinga.

“Wizara inawahimiza watu wote wenye dalili za magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa kama vile homa, mafua, kikohozi, mwili kuchoka, maumivu ya viungo, kuumwa kichwa kwenda vituo vya kutolea huduma za afya mapema ili kuweza kupimwa ni kupatiwa matibabu stahiki,”imesema taarifa ya Prof. Nagu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!