Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yamwinda Maalim Seif, CUF yang’aka
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yamwinda Maalim Seif, CUF yang’aka

Spread the love

VITA vya kisiasa ndani ya Chama cha Wananchi (CUF) vinawasogeza karibu viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na sasa wanampigia hesabu Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu wa chama hicho. Anaandika Faki Sosi … (endelea).

Chadema imeeleza kuwa, Maalim Seif atakuwa mgombea urasi wake kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 visiwani Zanzibar pale mgogoto wa chama hicho utaposhindwa kupatiwa ufumbuzi na chama hicho kuparaganyika.

Taarifa ya mwanasiasa huyo kuwindwa na Chadema kugombea urais visiwani humo kwenye uchaguzi mkuu ujao imetolewa leo tarehe 11 Septemba 2018 na Hashimu Juma, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Chadema.

Juma mesema kuwa, ndoto ya upinzani ni kushika dola na kwamba, CUF Zanzibar imeimarika kupitia Maalim Seif na kwamba, kwa upande wa Bara Chadema ndio iliyoimarika hivyo kwa umoja wa vyama hivyo viwili, malengo yao yatafikiwa.

Amesema kuwa, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa kikitumia mbinu chafu za kisaia kwa kuibua migogoro ndani ya vyama vya siasa nchini kama walivyokitibua chama cha CUF ya kukifanya kuwa na vipande viwili ili kisiweze kufanya operesheni yoyote ya kisiasa.

Juma amesema kuwa Chadema itampa nafasi Maalimu Seif ya kugombea nafasi ya urais ndani ya `chadema visiwani Zanzibar na huku wabunge wake wakiwa kwenye nafasi zao kwenye majimbo yao.

Amesema kuwa CUF hakina uwezo wa kusimamisha mgombe kwa sasa kutokana na mgogoro uliopandikizwa ndani ya chama hicho.

Mbarara Maharagande, Naibu Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano kwa Umma amesema kuwa, CUF hawana mpango uliotangazwa na chadema kwamba, Maalim Seif anaweza kugombea urais kupitia chama hicho.

“Si mpango wa CUF kuungana na Chadema kama ambavyo imeelezwa na Chadema, CUF itaendelea kusimama yenyewe na tutaendelea kushirikiana kwa mambo mengine kama ilivyo sasa,” amesema Mbarara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!