Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif: Wanataka kuni – Lissu
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif: Wanataka kuni – Lissu

Maalim Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamadi, mgombea urais visiwani Zanzibar amesema, Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) inataka kumfungia kama Tundu Lissu, mgombea urais Tanzania kupitia Chadema alivyofungiwa kufanya kampeni kwa siku saba. Anaandika Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Ni baada ya Kamati ya Maadili ya ZEC kumtaka kufika mbele yake leo tarehe 15 Oktoba 2020 kujibu tuhuma zilizowasilishwa na Chama cha Demokrasia Makini kwamba,  anashawishi wafuasi wake kupiga kura tarehe 27 Oktoba 2020 badala ya tarehe 28 Oktoba 2020.

“…nimetakiwa nifike Kamati ya Maadili ya ZEC. Eti nimelalamikiwa na Chama cha Demokrasia Makini kwa kuwaambia watu wakapige kura Oktoba 27.

Maalim Seif, M/kiti ACT-Wazalendo Taifa

‘Wanataka kuni-Lissu. Hawa wanatumika na CCM. Kama Mwinyi (Dk. Hussein Mwinyi, mgombea urais Zanzibar kupitia CCM) ana hoja akajibu jukwaani. Narudia sote tukapige kura Oktoba 27,” ameandika Maalim Seif.

Sheria ya Uchaguzi Zanzibar imeweka utaratibu kwa baadhi ya watumishi wa umma hasa wanaosimamia siku ya uchaguzi, kupiga kura siku moja kabla ya siku ya uchaguzi husika.

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!