Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif: Wanataka kuni – Lissu
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif: Wanataka kuni – Lissu

Maalim Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamadi, mgombea urais visiwani Zanzibar amesema, Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) inataka kumfungia kama Tundu Lissu, mgombea urais Tanzania kupitia Chadema alivyofungiwa kufanya kampeni kwa siku saba. Anaandika Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Ni baada ya Kamati ya Maadili ya ZEC kumtaka kufika mbele yake leo tarehe 15 Oktoba 2020 kujibu tuhuma zilizowasilishwa na Chama cha Demokrasia Makini kwamba,  anashawishi wafuasi wake kupiga kura tarehe 27 Oktoba 2020 badala ya tarehe 28 Oktoba 2020.

“…nimetakiwa nifike Kamati ya Maadili ya ZEC. Eti nimelalamikiwa na Chama cha Demokrasia Makini kwa kuwaambia watu wakapige kura Oktoba 27.

Maalim Seif, M/kiti ACT-Wazalendo Taifa

‘Wanataka kuni-Lissu. Hawa wanatumika na CCM. Kama Mwinyi (Dk. Hussein Mwinyi, mgombea urais Zanzibar kupitia CCM) ana hoja akajibu jukwaani. Narudia sote tukapige kura Oktoba 27,” ameandika Maalim Seif.

Sheria ya Uchaguzi Zanzibar imeweka utaratibu kwa baadhi ya watumishi wa umma hasa wanaosimamia siku ya uchaguzi, kupiga kura siku moja kabla ya siku ya uchaguzi husika.

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

error: Content is protected !!