Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif: Uvumilivu wetu umefika mwisho
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif: Uvumilivu wetu umefika mwisho

Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu wa chama cha wananchi CUF.
Spread the love

KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad amesema viongozi na wanachama wa chama hicho wapo tayari kwa lolote kutokana na uhujuma wanazofanyiwa na serikali, anaandika Shabani Matutu.

Maalim Seif amebainisha kuwa hajashindwa kazi, kama vibaraka wa serikali wanavyosema bali anaendelea kufanya kazi za chama hicho na muda si mrefu ataanza rasmi ziara yake jijini Dar es Salaam baada ya kumaliza ziara yake Zanzibar.

Maalim Seif amewambia wanahabari leo jijini Dar es Salaam kuwa sema kuwa amekuwa na ziara ya kuimarisha chama chicho katika kisiwa cha Unguja, hata hivyo ameamua kukatisha ili kuzungumza na Watanzania kutokana hali ya kisiasa iliyopo.

“Nataka ifahamike kuwa mgogoro wa kupandikizwa kwa kumtumia Profesa Ibrahim Lipumba hauna lengo la kuiua CUF bali upinzani na hasa Ukawa, ambapo lengo pana ni kuua demokrasia Tanzania kwa kuhujumu na kuzuia taasisi zote zinazooneka kuwa ni nguzo imara za demokrasia yetu,” amesema.
Amesema kuwa kuna mbinu mbalimbali ambazo zinatumika kuua demokrasia kwa kunyamazisha taasisi zinazothubutu kutoa mawazo tofauti na yale ya watawala walioingia madarakani mwaka 2015.

Maalim Seif amesema kuwa kupigwa marufuku kwa mikutano ya hadhara na maandamano ya vyama vya siasa nchi nzima. Kuzuiwa kwa matangazo mubashara ya mikutano ya Bunge ni miongoni mwa mbinu za uminyaji wa demokrasia hapa nchini.

Pia ameeleza juu ya kufinywa kwa bajeti ya shughuli za Bunge na hasa Kamati za Bunge ili zisiweze kufanya kazi ya kuisimamia serikali, kuchunguza mapungufu ya viongozi na watendaji wa serikali.

“Wanawakamata, kuwabughudhi, kuwalaza ndani na kuwafungulia mashtaka wabunge wa upinzani hasa wale wanaoonekana kuwa mwiba mkali kwa watalawa ili kuwatisha na kuwanyamazisha wasifanye kazi yao ya kuwakosoa watawala,” amesema.

Maalim amesema ghiliba za utawala uliopo madarakani zimefika mpaka katika mhimili wa mahakama ambapo serikali inatoa maagizo hadharani ya jinsi ya kuamua kesi na hata kuahidi kuwapa fedha wanazozihitaji kwa ajili ya uendeshaji wa mahakama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!