MAALIM Seif Sharif Hamad na Salim Biman, wapo njiani kuelekea Pemba kuitikia wito wa Jeshi la Polisi wilayani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).
Maalim Seif, Mshauri Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo na aliyewahi kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Bimani ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wanaitikia wito huo leo tarehe 14 Januari 2020, katika kituo cha Polisi Wilaya ya Wete.
Pamoja na kuitikia wito huo, hakuna taarifa zaidi zilizoelezwa kuhusu lengo la wito huo. MwanaHALISI Online linaendelea kufuatilia.
Leave a comment