Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif awakaribisha wanaotaka kumweka pingamizi
Habari za Siasa

Maalim Seif awakaribisha wanaotaka kumweka pingamizi

Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Mgombea Urais Zanzibar kupitia ACT- Wazalendo amewakaribisha wale wote ambao wanataka kumwekea pingamizi Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kufanya hivyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Unguja … (endelea).

Maalim Seif ametoa kauli hiyo jana Jumanne tarehe 8 Septemba 2020 alipozungumza katika Kongamano la Vijana wa ACT-Wazalendo visiwani humo.

Tayari Maalim Seif amekwisha kuchukua fomu za utezi wa kugombea urais ZEC katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 27 na 28 Oktoba 2020.

Fomu hizo amezirejesha leo Jumatano tarehe 9 Septemba 2020.

Amesema, kuna watu wa vyama vingine wamepanga kumwekea mapingamizi ZEC ili asiteuliwe kugombea.

Maalim Seif ambaye pia ni Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo anawakaribisha watu wanaotaka kumwekea pingamizi akisema anafahamu namna ya kupangua mapingamizi yao.

“Nasikia kuna watu washapangwa na vyama vingine kuniwekea pingamizi, nawakaribisha sababu kuniwekea pingamizi yeye anakuja kutoa haja zake na ushahidi wake na mimi naujua vilevile.”

“Sioni kama kuna pingamizi yoyote, kama itasimama juu yangu. Mimi nimezaliwa Mtambwe hamjui ninyi? Ndiyo sifa ya kwanza ya mgombea urais awe Mzanzibar wa kuzaliwa sio Mzanzibar mkaribishi,” amesema Maalim Seif.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za Siasa

Kamugisha aanika utekelezaji mpango kazi 2022/23

Spread the loveMWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo Mkoa...

Habari za Siasa

Vijana ACT-Wazalendo wakabidhiwa kivumbi kulinda kura uchaguzi 2024,2025

Spread the loveNGOME ya Vijana ya Chama cha  ACT-Wazalendo, imetakiwa kuwanoa wafuasi...

error: Content is protected !!