Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif aonesha njia ya ushindi 2020
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif aonesha njia ya ushindi 2020

Maalim Seif Shariff Hamad
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Mshauri Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo amesema, ushirikiano ndio njia muhimu ya kushinda kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Kutokana na hali hiyo amesema, ACT-Wazalendo wanahitaji ushirikiano na vyama vingine vya upinzani ili kukishinda Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Msimamo wa ACT-Wazalendo, tunaamini tunahitaji mashirikiano, hatuwezi kwenda kwenye uchaguzi huu chama kimoja kimoja.

“Mwaka 2015 kuna maeneo tulipoteza kwa kura chache, kwa kuwa kura ziligawika, wapinzani wangeungana CCM ingepoteza. Vyama vilivyo serious (makini) kuungana na kushirikiana ni jambo muhimu sana sana, tunahitaji kufanya kazi pamoja,” amesema Maalim Seif.

Amesema, tayari chama chao kimeanza taratibu kuhakikisha kunakuwa na ushirikiano kwenye uchaguzi huo, “ni mapema mno kusema tumefikia hatua gani, lakini response (mwitikio) tuliyoipata sio mbaya.”

Amesema, wananchi wana imani naye na kwa bahati nzuri kila uchaguzi kura zake zimekuwa zikiongezeka kwa kuwa anaaminiwa na Wazanzibari.

“Mimi ni mwanasiasa, kubwa wananchi wana imani name. Mara zote nagombea niliamini wananchi wana imani na mimi ndio maana ninashinda.

“Wakati wwt nitapoona imani ya wananchi imepotea, sintoendelea lakini sasa hivi kwa uchunguzi wetu, bado wananchi wana imani na mimi na sasa wanasubiri maamuzi yangu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!