Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif amvimbia Waziri wa JPM
Habari za Siasa

Maalim Seif amvimbia Waziri wa JPM

Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Mshauri Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, ‘amemvimbia’ Hamadi Massauni, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, kwamba hawezi kumzuia kufanya siasa Visiwani Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Maalim Seif ametoa kauli hiyo leo tarehe 13 Desemba 2019, siku moja baada ya Masauni kuagiza kushuswa vyeo Makamanda wa Jeshi la Polisi, Mikoa ya Kaskazini Pemba na Kusini Unguja.

Masauni aliagiza hivyo kwa madai, polisi hao wamefanya kosa la kumruhusu Maalim Seif afanye mikutano ya hadhara.

Akizungumzia hatua hiyo, Maalim Seif amesema, hakuna mtu wa kumzuia Zanzibar, na kwamba atakwenda popote atakapo.

“Nakwambia Masauni hakuna mtu wa kunizuia Zanzibar nitakwenda popote nitakapo ndani ya nchi yangu,” amesema Maalim Seif.

Makamanda walioshushwa cheo ni, Sheikhani Mohamedi Sheikhani, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba na Hassan Nassir Ally, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kusini Unguja.

Maalim Seif yuko Visiwani Zanzibar kwenye ziara ya kukusanya maoni ya wananchi, kwa ajili ya kuandaa ilani ya ACT-Wazalendo ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!