Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif amfuata JPM Ikulu
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif amfuata JPM Ikulu

Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Mshauri Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, ametinga Ikulu, jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo na Rais John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Muda mfupi baada ya kukutana na Rais Magufuli leo tarehe 3 Machi 2020, Maalim Seif ameeleza kuwa wamezungumzia masuala ya nchi na namna ya kufanya amani iendelee kuwepo.

“Tumekutana na kubwa tumezungumzia mambo ya nchi yetu, vipi tutaendelea kuifanya Tanzania iwe na amani, nchi ya salama na upendo kwa Watanzania wote,” amesema Maalim Seif na kuongeza:

“Ni mtu muwazi na anapenda kukutana na watu, nafurahi sana kwa rais anakubali kukutana na raia wake…, namshukuru rais kakubali tukutane, tuzungumze mambo ya maslahi ya nchi yetu.”

Hata hivyo, Maalim Seif ameeleza kwamba, mengine aliyoongea na rais yatabai ndani na hayawezi kupelekwa kwa jamii “mengine tumezungumza humo ndani mimi na rais, huwezi kuyasema public (wazi), bila shaka kukiwa na haja ya kukutana, tutakutana tena.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!