Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif ajitosa Serikali za Mitaa
Habari za Siasa

Maalim Seif ajitosa Serikali za Mitaa

Maalim Seif Shariff Hamad
Spread the love

MABADILIKO kamili katika siasa, uchumi na kijamii hayawezi kufikia iwapo wananchi watasita kwenda kujiandikisha ili kupiga kura. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Maalim Seif Sharif Hamad, Mshauri wa Chama cha ACT-Wazalendo leo tarehe 9 Oktoba 2019, siku moja baada ya zoezi la uandikishaji wapiga kura linaloendeshwa na Wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI kuanza.

Mwanasiasa huyo nguli na Katibu Mkuu wa zamani wa Chama cha Wananchi (CUF), amewataka Watanzania kujiandikisha ili wapate fursa ya kuchagua viongozi wapya kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa Nonemba mwaka huu, watakaoongoza katika kwa mitano (2019- 2024).

“Tujiandikishe tafadhari. Usikose kujiandikisha na kuwa sehemu na kushiriki kikamilifu kuleta maendeleo tuyatakayo Tanzania,” amesema Maalim Seif na kuongeza.

“Tumepata fursa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kufanya maamuzi ya kuchagua viongozi wapya katika kipindi cha miaka mitano. Tujiandikishe.”

Zoezi hilo linafanyika kwa muda wa siku saba, kuanzia tarehe 8 hadi 14 Oktoba 2019.

Uchaguzi wa serikali za mitaa unatarajia kufanyika mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka huu, ambapo Watanzania watachagua viongozi wa serikali wa vijiji, vitongoji na mitaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!