Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif afungiwa kufanya kampeni
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif afungiwa kufanya kampeni

Spread the love

KAMATI ya Maadili ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), imemfungia siku tano kutofanya kampeni, Maalim Seif Sharif Hamad, mgombea urais wa Zanzibar kuanzia kesho 16-20 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Hatua hiyo inatokana na Chama cha Demokrasia Makini kiliwasilisha malalamiko Maalim Seif ameshawishi watu wapige kura 27 Oktoba.

Kwa maana hiyo, Maalim Seif atakuwa amebakiza siku sita za kufanya kampeni kuanzia tarehe 21 hadi 26 Oktoba 2020 na siku inayofuata itakuwa ni kura ya awali na 28 Oktoba kura kwa wananchi wote.

Kilichomkuta, Maalim Seif ni kama kilichomtokea Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema aliyefungiwa na kamati ya maadili ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutofanya kampeni kwa siku saba.

Lissu alilalamiliwa na vyama vya NRA na CCM kwamba ametoa maneno ya uchochezi yaaiyoweza kuthibitishwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!