Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif afungiwa kufanya kampeni
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif afungiwa kufanya kampeni

Spread the love

KAMATI ya Maadili ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), imemfungia siku tano kutofanya kampeni, Maalim Seif Sharif Hamad, mgombea urais wa Zanzibar kuanzia kesho 16-20 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Hatua hiyo inatokana na Chama cha Demokrasia Makini kiliwasilisha malalamiko Maalim Seif ameshawishi watu wapige kura 27 Oktoba.

Kwa maana hiyo, Maalim Seif atakuwa amebakiza siku sita za kufanya kampeni kuanzia tarehe 21 hadi 26 Oktoba 2020 na siku inayofuata itakuwa ni kura ya awali na 28 Oktoba kura kwa wananchi wote.

Kilichomkuta, Maalim Seif ni kama kilichomtokea Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema aliyefungiwa na kamati ya maadili ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutofanya kampeni kwa siku saba.

Lissu alilalamiliwa na vyama vya NRA na CCM kwamba ametoa maneno ya uchochezi yaaiyoweza kuthibitishwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

error: Content is protected !!