Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Maalim Seif afikisha siku ya tisa hospitalini
HabariTangulizi

Maalim Seif afikisha siku ya tisa hospitalini

Maalim Seif Sharrif Hamad, Aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
Spread the love

 

MAKAMO wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, bado anaendelea kupata matibabu katika hospitali kuu ya Mnazi Mmoja, Visiwani Unguja. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Maalim Seif, amelazwa hospitalini hapo tangu tarehe 26 Januari 2021, akielezwa kuugua maambukizi ya virusi vya Corona (COVID-19).

Katibu wa Maalim Seif, Issa Kheri Hussein, ameeleza MwanaHALISI Online, jana Jumatano tarehe 3 Februari 2021, kuwa bado kiongozi huyo yuko hospitali akipatiwa matibabu.

“Mimi ni katibu wake private (binafsi) wa ofisi. Siyo msemaji wa masuala yake binafsi. Kwa sasa, nature (asili) yake ni Makamo wa Kwanza wa Rais na hivyo, taarifa zake ziwe authorised kutolewa (zitolewe na mamlaka). Lakini bado yupo hospitali, anaendelea na matibabu,” ameeleza Hussein.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar, Dk. Juma Mohammed, alipoulizwa maendeleo ya afya ya kiongozi huyo, haraka alisema, “sina mamlaka ya kulizungumzia.”

Taarifa kuwa Maalim Seif amelazwa hospitali kufuatia kuambukizwa virusi vya Covid-19, zilitolewa tarehe 31 Januari 2021 na Katibu Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo,  Ado Shaibu.

Ado alisema, Maalim Seif, mkewe Bi. Awena, pamoja na wanafamilia wake kadhaa, wamethibitika kuugua virusi hivyo.

Aidha, aliyepata kuwa waziri wa Afya katika serikali iliyopita ya Zanzibar, iliyoongozwa na Dk. Alli Mohammed Shein, Hamad Rashid Mohammed, alinukuliwa alisema, amejulishwa kuwa Maalim Seif yuko hospitali baada ya kushambuliwa na virusi vya Corona.

Waziri huyo wa zamani wa afya ambaye ni kiongozi wa chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), aliwataka wananchi kumuombea dua mwanasiasa huyo mkongwe Visiwani ili aweze kurejea katika majukumu yake.

Hata hivyo, pamoja na Maalim Seif, kuwa Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUKI), siyo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) wala Serikali ya Jamhuri ya Muungano, iliyotoa taarifa kuhusiana na ugonjwa wake

1 Comment

  • Jambo la ajabu na la kustaajabisha ni kuwa makamo wa rais yuko hospitali lakini serikali inakaa kimyaa na daktari wake wamekaa kimya.- usiri huu wa nini? Kiongozi wa taifa akipatwa ugonjwa wananchi hawapaswi kujua?
    Tunaambiwa na ACT kuwa ameambukizwa Corona. Je walijuaje? Alifanyiwa vipimo hapo hospitali? Majibu yalisemaje?
    Tuamini yanayosemwa na ACT wakati serikali na madaktari wake hawataki kutuambia?
    Mwalimu Nyerere aliwahi kusema
    “Hatuwezi kutatua matatizo yetu kwa kujidanganya kuwa hayapo”
    AIBU

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!