Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif aeleza tiba ajira za ubaguzi Z’bar
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif aeleza tiba ajira za ubaguzi Z’bar

Maalim Seif Sharrif Hamad, Aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, ameeleza kuanzishwa kwa mfumo mpya wa ajira ikiwa ni hatua za kutibu ubaguzi wa ajira visiwani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Amekiri kuwepo kwa ubaguzi wa ajira kwa baadhi ya Wazanzibari, unaotokana na misingi ya tofauti za kisiasa na kwamba, tatizo hilo linakwenda kupatiwa ufumbuzi.

“… kulikuwa na changamoto katika taasisi za kiserikali katika kuajiri, sasa serikali itaanzisha mfumo rasmi wa kimtandao kwa kuomba ajira na sio kama zamani,” amesema Maalim Seif wakati wa ziara yake kisiwani Pemba jana Jumatano tarehe 6 Januari 2021.

Kwenye ziara hiyo, Maalim Seif amesema, wananchi hususan vijana, wanatarajiwa kunufaika na uwekezaji ambao uko njia kufanyika katika uvuvi.

“Kuna uwekezaji unaotarajiwa kufanyika katika sekta ya samaki, uwekezaji huu utawanufaisha hususani vijana,” amesema.

Maalim Seif ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha ACT –Wazalendo, anaendelea na ziara yake Pemba akikutana na viongozi mbalimbali wa serikali, chama chake na wakuu wa taasisi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!