JESHI la Polisi Zanzibar, limemwachia kwa dhamana, mgombea Urais wa Zanzibar kupitia ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam …(endelea).
Maalim Seif ameachiwa leo jioni Jumanne tarehe 27 Oktoba 2020 na kutawakiwa kuripoti Jumatatu ijayo kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi kwa mahojiano zaidi.
Mwanasiasa huyo mkongwe, alikamatwa leo asubuhi katika Kituo cha kupigia kura cha Garagara visiwani humo, alipokwenda kupiga kura ikiwa ni siku ya kwanza ya upigaji kura wa Uchaguzi Mkuu wa madiwani, wabunge, wawakilishi na Rais utaohitimishwa kesho.
Leave a comment