Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Ma-DC wapya Dar wapewa majukumu matano
Habari za SiasaTangulizi

Ma-DC wapya Dar wapewa majukumu matano

Almas Nyangassa, Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni akiapa mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla
Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amewakabidhi majukumu matano wakuu wa wilaya za mkoa huo, walioteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan, tarehe 19 Juni 2021. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Makalla amekabidhi majukumu hayo, leo Jumatatu tarehe 21 Juni 2021, wakati akiwaapisha Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kherry James na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Fatma Almasi Nyangasa, ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Jukumu la kwanza ni ukusanyaji mapato, ambapo amewataka wakuu wa wilaya hao kusiammia ukusanyaji na matumizi ya mapato.

“Neno mkuu nimegawanya kwa vipaumbele, M ya kwanza ni mapato. Mkasimamie mapato, kila ukiniambia mkuu salama, kumbuka M ya kwanza ni mapato,”

“Ili Serikali iweze kuhudumia wananchi wake na ikafanya maendeleo lazima tuwe na mapato, mkasimamie mapato katika wilaya zenu, mkadhibiti mapato,” amesema Makalla.

Makalla ametaja jukumu la pili kuwa ni kutatua kero za wananchi wa maeneo yao.

“Jukumu lingine mkasikilize kero za wananchi, unaponiambia mkuu maana yake mkawe karibu na wananchi.  Msikilize kero za wananchi, watu wetu wana changamoto kuanzia chini, kwenye mtaa hadi halmashauri, wote tukasikilize kero za wananchi,” amesema Makalla.

Viongozi hao wapya, wameelezwa kwamba jukumu lao la tatu ni ulinzi na usalama, ambapo Makalla amewataka wakaunde mikakati madhubuti ya kupambana na uhalifu hasa wizi ulioibuka hivi karibuni wa vifaa vya magari.

Kheri James, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, akiapa mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla

“Nyie mnaenda kuwa wenyeviti wa kamati ya ulinzi na usalama, lazima tuhakikishe wananchi wetu wanakuwa salama katika maeneo yao.  Tupambane na uhalifu, sasa hivi kuna wimbi la wizi wa vifaa vya magari, mtu unaamka asubuhi gari halipo kila kitu kinakokotolewa,” amesema Makalla.

Makalla ametaja jukumu la nne kuwa ni usafi “nataka Dar es Salaam iwe safi, weka mikakati katika wilaya yako kusimamia usafi, Jiji la Dar es Salaam lazima liendelee kuwa taswria ya Tanzania.”

Mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam, ametaja jukumu la mwisho kuwa ni, usimamizi wa miradi ya maendeleo.

“Jukumu lingine la mwisho, usimamizi wa miradi ya maendeleo, tukasimamie kila mradi.  Uujue mradi uliopo katika eneo lako, uufuatilie na utekelezaji wake kwa kiwango kinachotakiwa,” amesema Makalla.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!