MAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote juu ya muda wa miaka 100 wa uwekezaji kwenye Bandari ya Dar es Salaam kupitia Kampuni ya DP World kutoka Falme za Kiarabu kama inavyoenezwa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Kauli hiyo ya Lissu imekuja siku moja baada ya kuibuka mjadala kuhusu uwepo wa mkataba wa kampuni hiyo kwamba inatarajiwa kuwekeza bandarini kwa miaka 100 – jambo ambalo limezua taharuki.
Akizungumza na Mtandao wa Chanzo Kikuu leo Jumatano, Lissu ambaye pia ni mwanasheria mbobevu amesema; “Wakati huu ambao Chadema itatoa taarifa kuhusiana na sakata hili, mimi kwa maoni yangu binafsi nasema kuwa sijaona mahali popote kunapoonyesha kuwa Kampuni ya DP World wamepewa ofa ya miaka 100 ya kuendesha Bandari yetu,” alisema Lissu.
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini Tanzania (TPA), jana Jumanne usiku walilazimika kutoa taarifa kwa Umma, juu ya uwapo wa kikundi cha watu walioamua kwa makusudi kupotosha kuhusiana na mchakato wa maboresho ya Bandari nchini yenye lengo la kufanya kazi zake kwa ufanisi.
Leave a comment