Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100
Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the love

MAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote juu ya muda wa miaka 100 wa uwekezaji kwenye Bandari ya Dar es Salaam kupitia Kampuni ya DP World kutoka Falme za Kiarabu kama inavyoenezwa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Kauli hiyo ya Lissu imekuja siku moja baada ya kuibuka mjadala kuhusu uwepo wa mkataba wa kampuni hiyo kwamba inatarajiwa kuwekeza bandarini kwa miaka 100 – jambo ambalo limezua taharuki.

Akizungumza na Mtandao wa Chanzo Kikuu leo Jumatano, Lissu ambaye pia ni mwanasheria mbobevu amesema; “Wakati huu ambao Chadema itatoa taarifa kuhusiana na sakata hili, mimi kwa maoni yangu binafsi nasema kuwa sijaona mahali popote kunapoonyesha kuwa Kampuni ya DP World wamepewa ofa ya miaka 100 ya kuendesha Bandari yetu,” alisema Lissu.

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini Tanzania (TPA), jana Jumanne usiku walilazimika kutoa taarifa kwa Umma, juu ya uwapo wa kikundi cha watu walioamua kwa makusudi kupotosha kuhusiana na mchakato wa maboresho ya Bandari nchini yenye lengo la kufanya kazi zake kwa ufanisi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za Siasa

Kamugisha aanika utekelezaji mpango kazi 2022/23

Spread the loveMWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo Mkoa...

Habari za Siasa

Vijana ACT-Wazalendo wakabidhiwa kivumbi kulinda kura uchaguzi 2024,2025

Spread the loveNGOME ya Vijana ya Chama cha  ACT-Wazalendo, imetakiwa kuwanoa wafuasi...

error: Content is protected !!