Saturday , 10 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Lukuvi amteua Polepole ujumbe Bodi ya NHC
Habari za Siasa

Lukuvi amteua Polepole ujumbe Bodi ya NHC

Spread the love

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ameteua wajumbe saba wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), akiwemo Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa kwa umma iliyotolewa tarehe 20 Mei 2019 na Lukuvi imewataja wajumbe hao wapya akiwemo, Immaculate Senje, Sauda Msemo, Martine Madekwe, Mhandisi Mwita Rubirya, Abdallah Mwinyimvua  na Charles Singili.

“Kwa mamlaka niliyopewa chini ya Aya ya 1 (1) (b) ya Jedwali lililoanzishwa chini ya kifungu cha 5(2) cha Sheria ya Shirika la Nyumba la Taifa sura 295, nimewateua wajumbe wa bodi kuanzia leo tarehe 20 Mei 2019,” inaeleza taarifa ya Lukuvi.

Waziri Lukuvi amefanya uteuzi huo kufuatia uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa Dk. Sophia Kongela uliofanywa na Rais John Magufuli hivi karibuni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!